M-Bet Tanzania kuwajaza zawadi mashabiki wa soka katika Fainali ya Mabingwa barani Ulaya kati ya Bayern Munich na Paris Sait-Germain

KAMPUNI ya michezo ya kubahatisha ya M-Bet Tanzania itaipamba fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kati ya Bayern Munich na Paris Saint- Germain  kwa kutoa zawadi mbalimbali kwa mashabiki wa soka watakaojibu maswali mbalimbali, anaripoti Mwandishi Wetu…

Timu hizo zitakutana kwa mara ya kwanza Jumapili (Agosti 23), mwaka huu kwenye uwanja wa Estadio da Luz wa Ureno wenye uwezo wa kuingiza watazamaji  64,642 na M-Bet imeandaa kumbi mbili, Samaki Samaki Mlimani City na Masaki ambapo watafunga ‘screen kubwa’  kwa ajili ya kuonyesha mpira huo.

Meneja Masoko wa kampuni ya M-Bet Tanzania, Allen Mushi.

Meneja Masoko wa Kampuni ya M-Bet Tanzania, Allen Mushi amesema kuwa, mbali ya kuendesha chemsha bongo inayolenga mechi hiyo na historia ya mashindano ya Champions League, pia burudani mbalimbali zitakuwepo kwa ajili ya kuburudisha mashabiki.

Mushi amesema kuwa, wamefanya hivyo ili kuwakutanisha mashabiki wa soka na mbali ya kuangalia mechi, pia watajumuika pamoja na kubadilishana mawazo.

“Hii ni moja ya mikakati ya M-Bet Tanzania kuwakutanisha mashabiki pamoja na kujumuika kuangalia fainali hiyo ambapo zawadi kama za mipira, jezi, fulana na nyinginezo nyingi zitatolewa kwa wataojibu maswali ya fainali ya mechi hiyo na historia ya Ligi ya Mabingwa ya Ulaya,”amesema Mushi.

Amesema pia kutakuwa na maswali yahusiyo kampuni yao ambayo imefanikiwa kutoa washindi wengi na kuwazawadia zawadi mbalimbali ambazo zimeweza kubadili maisha yao.

Karibu! Tovuti hii ya www.diramakini.co.tz imesajiliwa rasmi na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kupewa leseni namba TCRA/OCS-BL/0197/2020 chini ya Diramakini Business Limited iliyosajiliwa nchini Tanzania kwa ajili ya kukuhabarisha, kukuelimisha na kukupasha habari mbalimbali toka ndani na nje ya nchi. Je? Una habari,maulizo au tangazo, unataka kutupa ufadhili? Tuwasiliane; diramakini@gmail.com Asante.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news