BREAKING NEWS: Mgombea Mwenza CHADEMA anusurika kifo


Gari analotumia Salum Mwalimu ambaye ni Mgombea Mwenza wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CHADEMA limepata ajali eneo la Msoka Kata ya Ngogwa wakati wakiwa njiani kutoka kwenye mkutano Kahama. Wote waliokuwa kwenye gari hilo wametoka salama, taarifa ya CHADEMA imebainisha.
 Afisa Habari wa CHADEMA, Tumaini Makene kupitia ukurasa wake wa Twitter amesema gari alilokuwa anatumia Mgombea Mwenza wa Urais CHADEMA imepata ajali na wote waliokuwa kwenye gari hiyo ni wazima wa afya.

“Tunamshukuru Mungu kwa kuwaponya katika ajali hii mbaya wote waliokuwa kwenye gari hii inayotumiwa na mgombea wa kiti cha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Salum Mwalimu Juma Mwalimu,"Tumaini Makene ameeleza.

 

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news