Geita yaanzisha Kijiji Maalum chenye ukubwa wa ekari 100 kwa ajili ya maonyesho

Mkoa wa Geita kwa kushirikiana na Halmashauri ya Mji wa Geita umeanzisha Kijiji Maalum kwa ajili ya Maonyesho chenye ukubwa wa ekari 100 katika Mtaa na Kata ya Bombambili mjini Geita, anaripoti Robert Kalokola (Diramakini) Geita.
Moja ya jengo la utawala la Kituo cha Ukanda wa Mamlaka ya Uwekezaji Kiuchumi (EPZA) ambalo liko ndani ya Kijiji cha Maonyesho chenye ukubwa wa ekari 100.(Picha na Robert Kalokola/Diramakini).
 
Kijiji hicho kimetengwa kwa ajili ya maonyesho ya bidhaa za aina mbalimbali, teknolojia pamoja na huduma kwa sekta mbalimbali ikiwemo kilimo,madini na ujasiriamali.
Moja ya jengo la utawala la kituo cha Ukanda wa mamlaka ya Uwekezaji Kiuchumi (EPZA) ambalo liko ndani ya Kijiji cha Maonyesho chenye ukubwa wa ekari 100(Picha na Robert Kalokola/ Diramakini).
 
Akizungumza katika kikao cha wakuu wa wilaya kutoka Chato,Mbogwe na Geita waliotembelea kijiji hicho,Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel amesema, kijiji hicho kitakuwa na maeneo yenye huduma kama benki,wanyamapori,burudani,kumbi za mikutano pamoja eneo la maonyesho.

Ameongeza kuwa, kijiji hicho kimeanza kutumika rasmi mwezi huu kwa ajili ya Maonyesho ya Teknolojia ya Madini ambayo yameanza Septemba 17, mwaka huu na yanatarajiwa kuhitimishwa Septemba 27, mwaka huu.
Baadhi ya wachimbaji wadogo wadogo na wajasiriamali wa Mkoa wa Geita wakifuatilia mafunzo katoka semina inayotolewa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) katika ukumbi wa EPZA katika Maonyesho ya Teknolojia ya Madini mjini Geita. (Picha na Robert Kalokola/Diramakini).
 
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel amesema kuwa, eneo hilo litakuwa na majengo mbalimbali na maeneo ya vivutio vingine.

Amesema kuwa,kwa kuanzia,mwaka huu kwenye hayo maonyesho ya teknolojia ya madini wanyama kama simba na chui ili watu waweze kushuhudia wanyama hao.

Wakuu wa wilaya kutoka Wilaya ya Chato ni Mhandisi Charles Kabeho,Wilaya ya Mbogwe Matha Mkupasi na Fadhili Juma Mkuu wa Wilaya ya Geita ambao wamefika kwa ajili ya kushuhudia maonyesho hayo.

Mkuu wa Wilaya ya Geita, Fadhili Juma amewaomba wajasiriamali wanaopata semina katika kijiji hicho kutoka NBC kutumia mafunzo hayo kwa vitendo baada ya mafunzo ili yawasaidie kukuza vipato vyao.
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel akifafanua jambo katika mafunzo kwa wachimbaji na wajasiriamali wa Mkoa wa Geita. (Picha na Robert Kalokola/Diramakini).
 
Jengo la EPZA la utawala katika kijiji hicho linajengwa chini ya ufadhili wa fedha za uwajibikaji kwa jamii (CSR) kutoka Mgodi wa kuchimba Dhahabu wa Geita (GGML) kwa usimamizi wa Halmashauri ya Mji wa Geita.

Maonyesho ya teknolojia ya madini na uwekezaji katika Mkoa wa Geita yalikuwa yanafanyika katika kiwanja cha CCM Kalangalala kwa awamu mbili.

Hii ni awamu ya tatu ya maonyesho hayo ambayo yanafanyika kwa mara ya kwanza katika Kijiji cha Maonyesho kilichopo chini ya Halmashauri ya mji wa Geita ikiwa ni mojawapo ya miradi yake maalum ya uwekezaji kwa ajili ya kukuza mapato ya halmashauri hiyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news