Hawa ndiyo wateule wa EJAT

Kamati ya Maandalizi ya Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari (EJAT) kwa mwaka 2019 imetangaza  majina ya wateule  54 wanaowania tuzo hizo katika makundi 21. 

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) 2019, Kajubi Mukajanga,akizungumza wakati  wa kutangaza wateule ya Tuzo hizo. Kushoto ni Meneja  Programu wa MCT, David Mbulumi

Wateule hawa wametangazwa Septemba 17, 2020 baada ya Jopo la Majaji  lililokutana Jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba 08 hadi 14, 2020 kumaliza jukumu la kupitia kazi zilizowasilishwa kuwania tuzo hizo.  

Kati ya wateuliwa hao 25 ni  kutoka magazeti, tisa  kutoka redio , wanne kutoka runinga, Kati ya wateule hao, 24 ni wanawake  - saba wakiwa wanatoka kutoka kwenye magazeti, mmoja kwenye vyombo vya habari vya mitandaoni na 16 kutoka vyombo vya kieletroniki wakati  wateule wanaume  ni 30  ambapo 17  kati yao  ni wa magazeti na wanane ni wa vyombo vya eletroniki  na wanne wa vyombo vya habari vya  mitandaoni.  

Jopo la Majaji liliongozwa na Pudenciana Temba. Majaji wengine ni  Mohammed Kissengo, Imane Duwe, Khalfan Said, Mkumbwa Ally na Pili Mtambalike ambaye alikuwa katibu wa jopo hilo. 

Washindi wa  tuzo hizo watajulikana rasmi katika kilele cha Tuzo za EJAT kitakachokuwa  Septemba 28,2020 katika hoteli ya  Tanga Beach Resort,  mjini Tanga ambapo mgeni rasmi atakuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga   Mheshimiwa Martin Shigela.

Jumla ya kazi  450  ziliwasilishwa kwa EJAT 2019. Kati ya hizo 192   ni  kutoka magazeti wakati wanahabari wa redio na ruinnga waliwasilishwa kazi 250 na vyombo vya habari vya mitandaoni kazi  nane. 

Taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa Maandalizi ya EJAT, Kajubi Mukajanga imeeleza kuwa kwa waandaji wa EJAT – Baraza la Habari Tanzania na washirika , mwelekeo huu ni mzuri licha ya matatizo yaliyokuwepo kwa kuwa wanahabari wengi zaidi wanaenzi na kuthamani EJAT, ambayo safari hii ni ya mwaka wa 11, kama  kipimo muhimu  kwa umahiri wa uandishi wa habari. 

Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya EJAT ni Baraza  la Habari Tanzania ambalo ni Mwenyekiti, Wakfu wa Vyombo vya  Habari Tanzania (TMF), Taasisi yaHhabari ya Kusini mwa Afrika  tawi la Tanzania (MISA-Tan), Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake  Tanzania (TAMWA), Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari  Tanzania (MOAT), HakiElimu,  ANSAF, Umoja wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania  (UTPC) na SIKIKA. 

Ifuatayo ni orodha  ya wateule  kutoka vyombombali vya habari,

WATEULE WA EJAT 2019

1 Neema Goyayi AFM Radio Dodoma

2 Fatma Abdallah Chikawe AZAM TV Dar es Salaam

3 Amina Semagogwa Radio Kwizera Kagera

4 Sauli Gilliard Daily News Dar es Salaam

5 Editha Karlo Mtanzania Kigoma

6. Zuhura Juma Said Zanzibar Leo Zanzibar

7 Idi Juma Afya Radio Mwanza

8 Yohani Gwangway Radio SAUT Mwanza

9 Dominic Mrimi Radio SAUT Mwanza

10. Gwamaka Alipipi Nipashe Dar es Salaam

11 Halili Letea The Citizen Dar es Salaam

12. Alfred Lastek Mushi Habari Leo Dar es Salaam

13. Sanula Athanas Sanula Nipashe Dar es Salaam

14 Baraka Jailosi Messa Habari Leo Songwe

15. Asha Ahmed Omar Chuchu FM Zanzibar

16 Hilda Phoya Mlimani TV Dar es Salaam

17 Agnes J. Almasy ITV Dar es Salaam

18 Deogratias Damian Macha Fountain Radio Kilimanjaro

19 Kelvin Matandiko Mwananchi Dar es Salaam

20. Kareny Masasy Habari Leo Shinyanga

21 Evanc Ng’ingo Habari Leo Dar es Salaam

22 Anord Jovine Kailembo Radio Kwizera Kagera

23 Agnes Mbapu TBC1 Dar es Salaam

24 Adella Herry Tillya EFM Radio Dar es Salaam

25 Betty Tesha TBC Taifa Dar es Salaam

26 Khamis Suleiman Said Channel 10 Dar es Salaam

27 Jamaly Hashim Said Azam TV Dar es Salaam

28 Essau Kalukubila Radio Jamii Micheweni Pemba

29 Joseline Joseph Kitakwa TBC FM Dar es Salaam

30 Isidory Peter Mtunda Pambazuko FM Ifakara, Morogoro

31 Ashton Balaigwa Nipashe Morogoro

32 Faraja Sendegeya Azam TV Dar es Salaam

33 Adam G. Hhando CG FM Tabora

34 Kija Yunus Mohamed Clouds TV Dar es Salaam

35 Regina Kulindwa Radio Sauti Mwanza

36 Agnes Anderson AFM Radio Dodoma

37 Rehema Mwaikema Azam TV Mwanza

38 Husna Mohammed Khamis Zanzibar Leo Zanzibar

39 Rehema Goodluck  Mwananchi Dar es Salaam

40 Lucas Raphael Habari Leo Tabora

41 Marco Maduhu Nipashe Shinyanga

42 Sifa Lubasi Habari Leo Dodoma

43 Harriet Makweta Mwananchi Dar es Salaam

44 Godfrey Kahango Mwananchi Dar es Salaam

45 Rahma S. Ali Zanzibar Leo Zanzibar

46 James Kandoya The Guardian Dar es Salaam

47 James Kamala Daily News Dar es Salaam

48 Crispin Samson The Guardian Dar es Salaam

49 Hadija Omar Nassor Voice of Tabora Tabora

50 Aurelia Palali Kwizera radio Kagera

51 Abdul Kingo Nipashe Dar es Salaam

52 Muhidin Msamba The Guardian Dar es Salaam

53 Bakar Masoud Bakar Chuchu FM Zanzibar

54 Rajab Mustapha Mrope Pangani FM Pangani, Tanga

Makundi yaliyoshindaniwa ni :

1. Tuzo ya  Kuripoti Biashara Uchumi na Fedha 

2. Tuzo ya kuripoti Utamaduni na Michezo  

3. Tuzo ya Kuripoti Kilimo na Biashara ya Kilimo

4. Tuzo ya Kuripoti Elimu 

5. Tuzo ya Kuripoti Utalii na Uhifadhi 

6.  Tuzo ya Kuripoti Habari za Uchunguzi  

7. Tuzo ya Uandishi Habari wa Data

8. Tuzo ya Kuripoti  Haki za Bianadamu na  Utawala Bora

9. Tuzo ya Mpiga Picha Bora  

10. Tuzo ya Mpiga Picha Bora wa Runinga 

11. Tuzo ya Mchora Vibonzo Bora  

12. Tuzo ya Kuripoti  Jinsia  

13. Tuzo ya Kuripoti Wazee 

14. Tuzo ya Kuripoti Watoto   

15. Tuzo ya Kuripoti Usimamizi wa Mafuta, Gesi na Uchimbaji Madini

16. Tuzo ya Kuripoti Afya ya  Uzazi 

17. Tuzo ya Kuripoti Ubunifu wa Maendeleo ya Binadamu

18. Tuzo ya Kuripoti Athari za Kemikali kwa Afya na Mazingira

19. Tuzo ya Kuripoti  Usalama Barabarani  

20. Tuzo ya Kuripoti Hedhi Salama 

21. Tuzo ya Wazi


Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news