Maswali yaongezeka kutekwa kwa Maria na wasiojulikana

KUFUATIA kusambaa taarifa za kutekwa kwa kiongozi wa maandamano nchini Belarus, Maria Kolesnikova na watu wasiojulikana ikiwemo kukamatwa kwa wanaharakati wengi wa kisiasa nchini humo, imeendelea kuzua maswali mengi, huku onyo likitolewa.
Maria Kolesnikova

Msemaji wa Kamisheni ya Umoja wa Ulaya, Peter Stano amesema, umoja huo una taarifa kuhusu madai ya kutekwa kwa mwanaharakati huyo pamoja na wanaharakati wengine wa kisiasa.

Stano amesema,wanachokishuhudia ni mwendelezo wa ukandamizaji unaofanywa na mamlaka dhidi ya raia na kuelezea wasiwasi kuhusu kuendelea kwa hatua hizo zinazochukuliwa kwa mirengo ya kisiasa jambo ambalo amesema halikubaliki.

Taarifa za Maria Kolesnikova kutekwa na watu wasiojulikana katikati ya mji mkuu wa Belarus, Minsk na kumpakizwa kwenye gari zimenea zaidi ndani na nje ya Taifa hilo.

Kwa mujibu wa shirika huru la habari la Tut.By la Belarus kutoka nchini humo limeripoti kuwa, baada ya Maria kutekwa na kupakiwa kwenyeb gari, watu hao wasiojulikana waliondokana naye.


Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news