Mbaroni kwa tuhuma za kuiba Vespa ya Bakar Omar Saleh

 JESHI la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, limefanikiwa kumkamata, Ahmada Daud Mwita (26) mkazi wa Sogea kwa kosa la wizi wa Vespa, ambayo ni mali ya Bakar Omar Saleh (43) mkazi wa Sogea.

Kamanda wa Polisi mkoa huo, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Awadh Juma Haji ameyasema hayo kwa waandishi wa habari wakati akitoa taarifa za matukio ya wiki yaliyotokea katika mkoa huo, huko ofisini kwake Mwembemadema jijini Zanzibar.

Kamanda Awadh amesema, baada ya tukio la wizi kufanyika, Vespa hiyo ilifichwa kwenye nyumba inayomilikiwa na Khalifa Mussa huko Mpendae Unguja.

Amesema, inasadikika kuwa mtuhumiwa huyo baada ya kuiba Vespa hiyo aliamua kuificha mbali na makazi yake, ili kuzuia watu kumuona, na muhusika kuigunduwa mali yake ilipo.

Kamanda alieleza kuwa, ilipofika Septemba 4, mwaka huu, majira ya saa 03:30 asubuhi waliweza kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo akiwa na vespa hiyo maeneo ya Mpendae kwa Kificho.

Aidha,emesema upelelezi wa kesi hiyo unaendelea, na ukikamlika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news