Mgombea Urais Twalib Ibrahim Kadege:Ilani yangu inasema mperampera spidi, nikiingia Ikulu wala rushwa watanikoma

“Mimi ilani yangu inasema Mperampera spidi narudia chama chetu kinasema kipaumbele chake mperampera spidi, sisi UPDP, mkituchagua tu tukikaa ikulu kazi ya kwanza kabisa ndugu zangu nikupambana na wala rushwa kwa sababu rushwa ni adui wa haki;

Mgombea wa Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha United Peoples Democratic Party (UPDP) Twalib Ibrahim Kadege ameahidi endapo atachaguliwa kuwa rais basi siku za mwanzo wataanza kupambana na rushwa.

Ameyasema hayo wakati akizindua rasmi kampeni za chama hicho jana Septemba 19, katika wilaya ya Kilwa mkoani Lindi na kusema kuwa ilani ya chama chao inaeleza jinsi ya kupambana na rushwa huku kauli mbiu ya chama hicho ikiwa ni mperampera spidi.
"Haya yote tunayo yalalamikia yanatokana na radhi ya rushwa, nchi yeyote duniani ikiwa na rushwa wananchi wake wanadhoofika, hawajiamini, hawajieliwi kwa sababu ya rushwa hii ndio kero kubwa sana,"amesema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news