Mizengo Pinda: Karatu msidanganyike, mafiga matatu ndiyo yanaenda kuwavusha hapa, kura mpeni Dkt.Magufuli, Ubunge Daniel Awaki na madiwani wote CCM


Waziri Mkuu mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda akiwahutubia wananchi mjini Karatu katika mwendelezo wa kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 28, mwaka huu.

Mheshimiwa Pinda amewaambia wananchi wa Karatu wayapuuze madai yanayotolewa na wapinzani kwa mgombea Ubunge wao, Daniel Awaki kuwa hajui Kiingereza kwani Ubunge si Kiingereza na wala si lazima uwe na Degree bali ujue kujenga hoja kwa maendeleo ya wananchi, anaripoti Sophia Fundi (Diramakini) Karatu.

Amesema, Mgombea huyo ana uwezo mzuri wa kujenga hoja na anaamini kupitia yeye chini ya uongozi wa Rais Dkt.John Magufuli na madiwani wa CCM, Karatu inakwenda kung'ara kila sekta baada ya Oktoba 28, mwaka huu.

"Hivyo niwaombeni ikifika siku ya kupiga kura, kura zote mpeni Mgombea Urais, Mheshimiwa John Magufuli, Mbunge Daniel Awaki na madiwani wote wa CCM, mtayafurahia maendeleo na hakika msikubali kudanganywa kwa hoja ambazo hazina mashiko,"amesema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news