TANESCO YATOA ELIMU KWA WACHIMBAJI WADOGO NA VIWANDANI

Mhandisi wa Umeme kutoka TANESCO, Hassan Kipende wa Idara ya AMR mita akieleza jambo wakati wa ukaguzi wa miundombinu ya shirika hilo mkoani Pwani.

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limeendelea na kampeni ya kutoa elimu juu ya matumizi bora ya umeme pamoja na kukagua miundombinu ya umeme na mota zinazotumiwa kwenye kuendesha mashine kwa wamiliki wa viwanda, machimbo ya madini na mashine za kusaga Mkoa wa Pwani, anaripoti NEEMA MBUJA.

Miongoni mwa elimu iliyotolewa ni pamoja na, namna ya kutumia vifaa ambavyo vinatumia umeme kidogo, umuhimu wa kukagua mota zao mara kwa mara kwa ajili ya kuleta ufanisi na usalama wa miundombinu.

Kuhusu wachimbaji wadogo wa mawe eneo la Chalinze, Mhandisi Hassan Kipende aliendelea kuwapatia elimu ya umuhimu na faida ya kutumia umeme kwani wengi wao bado wanatumia mafuta kuendesha mitambo ya kuchakata mawe jambo ambalo ni hasara kwao.

Akizungumza na wamiliki wa viwanda kwenye wilaya za Chalinze, Kibaha na maeneo ya Mlandizi mkoani Pwani, Mhandisi wa Umeme kutoka Idara ya AMR mita, Hassan Kipende amesema kuwa, kwa sasa baadhi ya viwanda vinatambua umuhimu wa kufunga 'power factor' ingawa baadhi bado hawajatambua umuhimu wake. Zinazofanana soma hapa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news