Waziri Biteko:Nishati ya umeme imekuwa chachu ya kuongeza ufanisi katika uchimbaji madini, hongereni TANESCO

Waziri wa Madini,Doto Biteko amesema kuwa uwekezaji uliofanywa na Shirika la Umeme nchini (TANESCO) katika Mkoa wa Geita umesaidia kuleta ufanisi katika shughuli za uchimbaji madini,anaripoti Robert Kalokola,Geita.

Biteko amelipongeza shirika hilo kwa kufikisha umeme kwenye maeneo ya uchimbaji dhahabu katika Mkoa wa Geita hususani maeneo ya wachimbaji wadogo  .
Waziri wa Madini, Doto Biteko (wa pili kushoto) akisikiliza maelezo kutoka kwa Ramadhan Kidunda ambaye ni Mhandisi wa Mradi wa TANESCO wa Bulyanhulu-Geita,Wengine ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel mwenye shati nyekundu. (Diramakini).

Waziri Biteko ameyasema hayo leo alipotembelea banda la TANESCO katika Maonesho ya Teknolojia ya Uchimbaji Madini yanayoendelea katika Kijiji Maalum cha maonyesho katika mji wa Geita mkoani hapo.

"Nishati ya umeme imekuwa chachu ya kuongeza ufanisi katika uchimbaji madini,"amesema Waziri  Biteko. 

Septemba 18, mwaka huu TANESCO iliwasha kituo chake kikubwa (Substation) cha kupozea na kusambaza umeme cha Mpomvu Mjini Geita kinachopokea umeme wa Kilovoti 220 kutoka Bulyanhulu.
Moja ya transfoma inayotumika kupoza umeme katika Kituo cha Mpomvu mjini Geita.(Diramakini).

Umeme unaotoka katika kituo hicho unasambazwa katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Geita ambao kwa mujibu wa TANESCO umemaliza tatizo la uhaba wa umeme katika mkoa huo.

Moja ya maeneo yanayonufaika na umeme huo ni kwenye migodi ya wachimbaji wadogo ndani ya Mkoa wa Geita.

Katika ziara hiyo, Waziri Biteko aliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Gabriel Robert, viongozi na wataalam mbalimbali  kutoka Wizara  ya Madini.

Maonyesho ya Teknolojia ya Uchimbaji Madini yalianza Septemba 17, mwaka huu na yatahitimishwa Septemba 27, mwaka huu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news