Rais Trump adai Democrat wamefanya ufisadi wa kura

Rais Donald Trump wa Marekani amedai kufanyiwa wizi katika uchaguzi mkuu wa taifa hilo pasipo kuwa na ushaihidi wowote. Amesema wapinzani wake wa Chama cha Democratic wanafanya jaribio la wizi katika uchaguzi huo ambao alidai yeye anaweza kushinda kwa urahisi dhidi ya Joe Biden, anaripoti Mwandishi Diramakini.

Trump ameyasema hayo katika Ikulu ya Marekani na kunukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari akisisitiza kuwa, "Kama ukihesabu kura halali, nitashinda kwa wepesi. Lakini kama utahesabu kura zisizo halali, wanaweza kutuibia uchaguzi huu".Kwa sasa timu ya Trump imeanzisha madai katika mamlaka husika kwa lengo la kukabiliana na kile Rais Trump alichokiita ufisadi wa chama cha Democrat. 

Aidha,maafisa katika baadhi ya majimbo ya uchaguzi bado hawajatoa uamuzi kuhusu malalamiko hayo. Lakini katika maeneo ya kuhesabu kura kama jimbo la Pennsylavania ambapo zaidi ya asilimaia 94 za kura zimehesabiwa Trump ana asilimia 49.7 na Biden 49.0. 

Kwa upande wa Jimbo la Arizona ambako asilimia 90 zimehesbabiwa Trump ana asalimia 48.5 na Biden 50.1, Georgia asilimia 99 zimehesabiwa Trump asilimia 49.4 na Biden asilimia 49.4 na Nevada kati ya asilimia 89 zilizohesabbiwa Trump asilimia 48.5 na Biden 49.4.

Wakati huo huo, Waafrika wengi wanaendelea kufuatilia matokeo ya uchaguzi mkuu wa Marekani kwa hisia tofauti zilizojaa kejeli na hali ya kutoamini hasa baada ya Rais Donald Trump kujaribu kujitangaza mshindi wa uchaguzi huo kabla ya hesabu ya kura kukamilika.

Katika baadhi ya nchi za Afrika ambazo uchaguzi umefanyika hivi karibuni na kukumbwa na utata wa matokeo kama Guinea, baadhi ya raia wameeleza kusikitishwa na Rais Trump kudai ushindi wakati hata hesabu ya kura ilikuwa inaonyesha kwamba alikuwa nyuma ya Joe Biden.

Mory Keita, ambaye ni raia wa Guinea amesema kwamba, Rais Trump anaonyesha mfano mbaya sana kwa nchi za Afrika ambazo bado ni changa kidemokrasia, huku Bachir Diallo akisema kuwa hatua ya Trump ni ya kuleta fedheha sana kwamba hayo ni mambo ambayo yanatarajiwa kutokea katika nchi yenye utawala mbovu sana na wala sio Marekani.

Kura zinaendelea kuhesabiwa katika uchaguzi wa Marekani, Joe Biden akiwa anaongoza kwa idadi ya kura, lakini hakuna mshindi amepatikana hadi sasa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news