Tetesi:Manchester City, Barcelona na Juventus zaelekea Borussia Monchengladbach

Klabu ya Arsenal kwa mujibu wa Mail inajiandaa kujadili kuhusu kuongeza mkataba wa kiungo wa kati wa Misri Mohamed Elneny (28) aliyewavutia tangu mwanzo wa msimu. 

Wakati huo huo, Express inaripoti, mmiliki wa Tottenham, Daniel Levy ametoa ofa kwa mshambuliaji, Son Heung-min (28) ya mshahara sawa na nahodha, Harry Kane likiwa ni jaribio la kuhakikisha kuwa mchezaji huyo wa Korea Kusini anasalia katika klabu hiyo. 

Bild inaripoti kuwa, Klabu ya Bundesliga, Schalke inaweza kuridhia kumruhusu beki wa kati Mturuki Ozan Kabak (20) kuondoka kwa pauni milioni 18 mwezi Januari, mwakani. Ingawa mabingwa wa England, Liverpool wanamuhitaji mchezaji mwenzake, Malick Thiaw (19).
Mshambuliaji wa Borussia Monchengladbach, Alassane Plea. (Gettyimages / Oliver Hardt). 

Pia klabu kubwa za Ulaya zikiwemo Manchester City, Barcelona na Juventus, zinamfuatilia washambuliaji wa Borussia Monchengladbach, Marcus Thuram (23) na Alassane Plea (27).

Kwa mujibu wa AS, Real Madrid huenda wakamsajili kiungo wa kati, Mfaransa Paul Pogba (27) kutoka Manchester United kwa kitita cha pauni milioni 54 msimu ujao.Pia MEN inaripoti kuwa,Manchester United imezungumza na kocha wa zamani wa Tottenham, Mauricio Pochettino kuhusu kuchukua nafasi ya Ole Gunnar Solskjaer.

Star inabainisha kuwa, nafasi ya Solskjaer iko katika hatihati baada ya vipigo vya mfululizo na anaweza kufukuzwa ikiwa United itapoteza kwa Everton siku ya Jumamosi.Kocha wa Manchester United kwa mujibu wa Sky Sports, anapata uungwaji mkono wa bodi na bado anatazamwa kama mtu mwenye ajira ya muda mrefu Old Trafford.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news