ZEC yawatangaza Wajumbe wa Viti Maalum vya wanawake

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) imewatangaza wajumbe 18 kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa nafasi za Viti Maalum vya Wanawake vya Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, anaripoti Jaala Makame Haji  (ZEC).
Tume imetangaza majina ya wajumbe hao katika mkutano wake uliofanyika leo Novemba 7, 2020 katika ukumbi wa mikutano wa tume hiyo uliopo Maisara jijini Zanzibar.

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar imewatangaza wajumbe 18 kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa mujibu wa masharti na maelekezo ya Ibara ya 67 ya Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984.

Aidha, tume imewatangaza wajumbe hao baada ya kuridhika kuwa wote wana sifa ya kuwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar kama zilivyoainisha katika Katiba ya Zanzibar Ibara ya 68.

Waliotangazwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar ni;

1. Bi.Panya Ali Abdallah

2. Bi. Bihindi Hamad Hassan

3. Bi.Salma Mussa Bilal

4. Bi.Shadya Mohammed Suleiman 

5. Bi.Fatma Ramadhan Mohamed (Mandoba)

6. Bi.Saada Ramadhan Mwenda

7. Bi.Mwantatu Mbaraka Khamis

8. Bi.Zainab Abdalla Salum

9. Bi.Riziki Pemba Juma

10. Bi.Leila Mohamed Mussa

11. Bi.Salha Mwinyi Juma

12. Bi.Hudhaima Mbarak Tahir

13. Bi.Sabiha Fil fil Thani

14. Bi.Aza Januar Joseph

15. Bi.Mwanaid Kassim Mussa

16. Bi.Mgeni Hassan Juma

17. Bi.Mwanajuma Kassim Makame 

18. Bi.Rahma Kassim Ali.

Hata hivyo, tume tayari imeshawasilisha majina ya Wajumbe hao kwa Katibu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar kwa ajili ya hatua nyingine za kisheria.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news