NA MWANDISHI DIRAMAKINI
WATANZANIA wametakiwa kujitokeza kuwasaidia watoto wenye mahitaji maamlumu wakiwemo yatima na wasiokuwa na walezi ili waweze kupata baraka zaidi katika maisha yao ya kila siku.

Amesema kuwa, Watanzania wamekuwa nyuma kwenye masuala ya kusaidia jamii, lakini kwenye shughuli za kuchangia harusi na sherehe mbalimbali wamekuwa wakijitokeza jambo ambalo wakati mwingine halina tija kwa jamii.
Pia amewataka warembo na wanamitindo wengine kuungana naye kuwawezesha wenye mahitaji maalum ili kuweza kutokomeza umasikini unaowasumbua watoto hao katika maeneo mbalimbali nchini.

Odemba amewaomba wafadhili wengine nchini na nje ya nchi kujitokeza kuwaunga mkono taasisi yake kwa kuwapa masaada ili kuendelea kusaidia watu wenye mahitaji maalum.
Kwa upande wake Msimamizi Mkuu wa kituo cha Salvation Army ,Bw. George Mbegani Mwasenga amesema kuwa, ujio wa Yaasisi ya Miriam Odemba imekuwa faraja kubwa kwa watoto hao wenye mahitaji maalum na kuwaomba watanzania wengine kujitokeza kwenda kuwatazama.

Aidha amesema kuwa kituo hicho kinakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo kuwama kwa baadhi ya mambo ambayo ni mahitaji maalum kwa watoto hao kutokana na gharama kuwa kubwa.