NA FRED KIBANO
SERIKALI imeridhishwa na ujenzi wa kituo cha afya Mtama katika Halmshauri ya Wilaya ya Mtama mkoani Lindi na kwamba waendelee kuzingatia ubora wanaotumika katika ujenzi wao.
Pia amebaini wanazingatia ubora unaotakiwa na hivyo amewaasa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo na watendaji wake kuendelea kusimamia ubora hasa katika hatua za umaliziaji ili majengo yasipoteze thamani yake.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mtama, Bw. George Mbilinyi amesema wanatarajia kukamilisha majengo yote matatu kwa wakati na kwamba endapo watapatiwa fedha za awamu ya pili kituo hicho kitapiga hatua kubwa ya miundombinu kuelekea kutoa huduma za afya kwa wananchi wa Mtama.
Amesema, kiasi cha fedha kilichotumika mpaka sasa ni shilingi 112,172,991 na salio shilingi 137,827,009 fedha zinazofanya kazi ya umaliziaji.