NA MWANDISHI DIRAMAKINI
Wanawake wameendelea kuonyesha ushujaa katika soka la Kimataifa baada ya kuendelea kuitoa kimasomaso Tanzania katika anga la Kimataifa.
Mabao ya Tanzanite leo yamefungwa na Mwamvua Haruna dakika ya 60 kwa penalti, Clara Luvanga dakika ya 80 na Emiliana Isaya dakika ya 83.
Aidha, Tanzanite iliyoshinda 1-0 dhidi ya Eritrea Jumamosi iliyopita bao pekee la Clara Luvanga dakika ya 90 itashuka tena dimbani Jumatano kumenyana na Ethiopia, kabla ya kuivaa Uganda Jumamosi na kukamilisha mechi zake kwa kucheza na Djibouti Novemba 9, mwaka huu.
Tags
Michezo