NA MWANDISHI DIRAMAKINI
MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa angalizo la mvua kubwa kwa baadhi ya maeneo ya mikoa ya Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Dar es salaam na Lindi pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.
TMA ni taasisi mahususi na pekee katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yenye Mamlaka ya kutoa huduma za Hali ya Hewa ndani ya Mipaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Makao Makuu ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania yapo jijini Dar es salaam, aidha mamlaka inatoa huduma zake pia kupitia vituo vyake vilivyopo katika maeneo mbalimnali mikoani.