NA GODFREY NNKO
MIEZI kadhaa ikiwa imepita baada ya uongozi wa Klabu ya Simba kuingia makubaliano ya kimkataba na Kampuni ya Vunja Bei wenye thamani ya shilingi bilioni 2 ya kutengeneza na kuuza jezi kwa kipindi cha miaka miwili, wametoa onyo kali kwa watu ambao wamekuwa wakijihusisha na uuzaji au usambazaji wa jezi zenye nembo yao ambazo hazijasambazwa na mzabuni.
Gonzalez alisema kuwa, mkataba huo utakuwa umempa nafasi ya kuuza bidhaa zote zinazohusiana na Simba kama jezi, kofia, soksi na vifaa vingine vya klabu hiyo.
Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa Vunjabei Group Limited, Fred
Fabian Ngajiro maarufu kama Fred Vunjabei aliishukuru klabu ya Simba kwa kuichagua kampuni hiyo kwa sababu kulikuwa na makampuni mengi, lakini waliamua kuipa nafasi kampuni yao kwa kuthamini ubora wa kazi zao.
Pia aliwaomba mashabiki wa Simba kuanza utaratibu wa kununua bidhaa rasmi za klabu ili kupata vifaa halisi na vyenye ubora mkubwa.