*Matukio muhimu ya kuenzi tunu, urithi, mawazo na mchango wake thabiti alioutoa kwa taifa kuratibiwa
NA FRESHA KINASA
KATIKA kuadhimisha kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa kwa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere itakayofanyika Aprili 13, 2022 eneo la Mwitongo Wilaya ya Butiama Mkoa wa Mara kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii wamejipanga kufanya matukio mbalimbali muhimu ya kuenzi tunu, urithi, mawazo na mchango wake thabiti alioutoa kwa taifa.
Rais wa Kwanza wa Tanzania, hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. ( Picha na Butiama Gallery/Govt).

Ambapo wadau mbalimbali zikiwemo taasisi za umma, binafsi na wananchi kwa pamoja wameaswa kushiriki katika kuenzi mema yote yoliyofanywa na Hayati Mwalimu Nyerere kwa manufaa endelevu ya nchi.
Oganga amebainisha kuwa, Mkoa wa Mara ni mdau namba moja katika kufanikisha jambo hilo, hivyo mkoa umejipanga vyema kwa kushirikiana na wizara hiyo pamoja na wadau wote kufanikisha kwa ufanisi huku akibainisha kuwa, matukio mengi muhimu ya kukumbuka mchango wa Baba wa Taifa yatakuwa yakiendelea kabla ya kufikia Aprili 13, 2022.

"Tutafanya matukio muhimu kabla ya Aprili 13, siku yenyewe na hata baada ya maadhimisho hayo hii yote ni katika kuenzi mchango wa Mwalimu Nyerere katika masuala mbalimbali kwa nchi yetu, wananchi na taasisi zina nafasi ya kushiriki kikamilifu kuona namna gani Mwalimu aligusa sekta husika,"amesema Dkt.Ntandu.

"Mwalimu Nyerere alikuwa mwanzilishi wa uhifadhi, tunatambua vyema tamko alilolitoa mwaka 1961 Mwalimu alitoa tamko la uhifadhi, wizara imeendelea kumuenzi Mwalimu kwa kuendelea kutoa elimu ya uhifadhi kwa jamii, hifadhi za Wanyamapori zimeongezeka nchini, mapori tengefu, na mengine kupandishwa hadhi kuwa mapori ya akiba.
Tags
Habari
Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere
Kumbukumbu
Maliasili na Utalii
Miaka 100 ya Mwalimu Nyerere
Mkoa wa Mara