
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia ( Sera, Bunge na Uratibu), Mhe. Ummy Nderiananga akifafanua jambo wakati wa kikao cha kujadili Bajeti ya Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA) katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera, Bunge na Uratibu), Bw. Kaspar Mmuya (wa kwanza kulia) akieleza jambo katika kikao hicho na (katikati) ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Balozi. Dkt. Pindi Chana na anayefuata ni Naibu Waziri wake, Mhe. Mhe. Ummy Nderiananga kikao kilichofanyika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome jijini Dodoma.

Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Dkt. Leonard Maboko akichangia hoja wakati wa kikao cha kujadili Bajeti ya Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome jijini Dodoma.

Kamishina Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Bw. Gerald Kusaya akichangia hoja wakati wa kikao cha kujadili Bajeti ya Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome jijini Dodoma.

Baadhi ya washiriki waliohudhuria kikao cha kujadili Bajeti ya Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA) wakifuatilia kikao hicho katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome Jijini Dodoma.(Picha na OWM-Sera,Bunge na Uratibu).