NA DIRAMAKINI
BENKI ya Akiba Commercial imesema kuwa, inatambua na kuheshimu imani za wateja na wadau wake popote pale walipo nchini.


"Tunaupa umuhimu wa kipekee sana mwezi mtukufu wa Ramadhan sio tu kwa wateja na wadau bali ni kwa waislamu wote, kwani kama benki tunathamini na kujali kila dini, hivyo tumejikita kikamilifu katika mwezi huu wa Ramadhan kwa ajili ya kuwashika mkono ndugu zetu Waislam,"amesema.
Akiba Commercial Bank, imekuwa na utaratibu wao kama benki yenye kujali na kutambua umuhimu wa mwezi huu mtukufu wa Ramadhan kwa kuwaruhusu wafanyakazi kutoka kazini mapema kwa ajili ya ibada na matayarisho ya futari.

Pia Akiba Commercial Bank, imekuwa na utaratibu wakufanya hafla ya kuandaa futari kwa wateja wao kila mwaka kwa ajili ya kuwaunga mkono Waislamu katika funga yao pia kudumisha mahusiano kati ya wateja na benki yao pendwa.