NA FRESHA KINASA
WANANCHI wa Kijiji cha Marasibora Kata ya Kisumwa Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara, wamepongeza hatua ya Chama cha Msalaba Mwekundu (Tanzania Red Cross Society)Mkoa wa Mara kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kutoa elimu ya utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji katika maeneo yao.


Neema Ogori amesema, awali hakuwa na ufahamu thabiti, kama kufanya shughuli za kilimo karibu na vyanzo vya maji kunachangia vyanzo kukauka. Ambapo kwa sasa elimu aliyoipata amesema atashiriki vyema katika kulinda vyanzo na kuwaelimisha wengine.

Paul Julias ameomba elimu ya utunzaji wa mazingira iendelee kutolewa maeneo mbalimbali kusudi wananchi wazidi kufahamu kwa upana zaidi faida za utunzaji wa mazingira na uzingatiaji wa sheria za mazingira.

Pia amewahimiza kuendelea kutoa elimu ya utunzaji wa mazingira kwa wananchi wengine, huku akisisitiza kuwa shughuli za kibinadamu zinapaswa kufanywa kwa kusingatia utunzaji wa mazingira kwa ajili ya kulinda maisha ya viumbe hai.

Pia, Nyalusi amewahimiza kupunguza taharuki pindi majanga yanapotokea na kutafuta njia sahihi za kuyashughulikia sambamba na kuzingatia utaratibu wa utoaji taarifa katika mamlaka za Serikali kupitia vijiji,mitaa, kata na wilaya.