NA SOPHIA FUNDI
WENYEVITI wa mamlaka ya mji mdogo wa Karatu mkoani Arusha wametakiwa kuwahamasisha wananchi kushiriki katika matukio mbalimbali ya kitaifa yanayoendelea ikiwemo zoezi la anwani za makazi pamoja na zoezi la chanjo ya polio inayoendelea kufanyika nchini.

Msigwa alisema kuwa, mwenyekiti wa kitongoji ni kiungo muhimu katika matukio yanayoendelea hivyo ni jukumu lao kushirikiana na wataalam wanaopita katika maeneo yao kwa ajili ya anwani za makazi ambapo alisema endapo zoezi hilo litakamilika vizuri litarahisisha zoezi la sensa linalotarajiwa kufanyika mwezi Agosti, mwaka huu.

Kwa upande wake mwenyekiti wa mamlaka ya mji huo, Yuda Morata aliwaomba wenyeviti kushirikiana na wataalam wanaopita kwenye maeneo yao kwa kuanisha maeneo yatakayowekwa vibao kwa kutoa elimu kwa wadau mbalimbali na wananchi.