NA FRESHA KINASA
SERIKALI mkoani Mara imesema inatambua kwa dhati mchango mkubwa unaotolewa na sekta binafsi mkoani humo katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya Mkoa na Taifa kwa ujumla.

Dkt. Haule mesema, sekta binafsi inachangia kwa kiwango kikubwa katika kutoa ajira, ulipaji wa kodi za maendeleo serikalini, kufanya miradi mbalimbali ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Huku akisema wazalishaji wakubwa na wafanyabiashara wakubwa nchini, wanatoka sekta binafsi.
Dkt. Haule mesema, maendeleo na uchumi wa Taifa unachangiwa kwa kiwango kikubwa na sekta binafsi. Huku akiitaka TCCIA kuendelea kuchagiza uanzishaji wa viwanda vidogovidogo vya kuongeza thamani na kusindika mazao ya kilimo, ufugaji na uvuvi pamoja na kutafuta masoko kwa ajili ya wazalishaji hao ili waweze kuuza kwa tija.

Ndengo amesema, mpango mkakati huo umebainisha fursa na rasilimali nyingi zinazopatikana mkoani Mara kupitia shughui za Uwekezaji, Utalii na Biashara.
Amezitaja baadhi ya fursa na rasilimali hizo kuwa ni ardhi nzuri kwa uzalishaji, maji ya kutosha ya Ziwa Victoria, watu, mifugo mingi, Mpaka wa Sirari, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Historia ya mkoa wa Mara kupitia Makumbusho ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Akielezea mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha mwaka uliopita 2021, Ndengo amesema, umoja huo umeweza kuzalisha wajasiriamali mahiri ambao wanalipa kodi kwa maendeleo na uchumi wa Taifa.

Akielezea miradi ya kimkakati ambayo ikikamilika itakuwa na tija kubwa katika uchumi na maendeleo ya mkoa wa Mara ni pamoja na ujenzi wa uwanja vya ndege Musoma na Serengeti.
Miradi mingine ni ujenzi wa Soko la Afrika Mashariki katika mpaka wa Sirari wilayani Tarime na Mpaka wa Kilongwe wilayani Rorya, kukamilika kwa ujenzi wa chuo kikuu cha Mwalimu Nyerere na ujenzi wa vyuo vya mafunzo ya ufundi Stadi VETA katika kila halmashauri.
Naye Mwenyekiti wa Wamachinga mkoa wa Mara, Charles Waitara amesema,wamachinga bado wanakabiliwa na changamoto ya uhaba wa mitaji, kwani hawana dhamana ya kuwawezesha kupata mikopo katika taasisi za fedha ambazo zinahitaji mkopaji awe na nyaraka za Usajili na dhamana.
Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Wafanyabiashara Wanawake Mkoa wa Mara, Judith Maganja Lugembe amesema, wanawake wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na maeneo ya kufanyia shughuli za uzalishaji.
Lugembe ameiomba Serikali kupitia Shirika la Viwanda Vidogo nchini (SIDO) kuongeza majengo na maeneo kwa wazalishaji wasiokuwa na maeneo ya kufanyia kazi zao.