NA DIRAMAKINI
MKUU wa Mkoa wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Amos Makalla ameelekeza Jeshi la Polisi kuanza mara moja msako wa kuwakamata watuhumiwa wa wizi na unyang'anyi kwa kutumia silaha maarufu kama Panya Road na kuwachukulia hatua kali za kisheria.

Hali hiyo ndio imemlazimu RC Makalla kuhitisha kikao kazi cha kukabiliana na uhalifu huo kikihusisha na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa, Wilaya, Wakuu wa Usalama, Makamanda wa Wilaya zote za Kipolisi, Wakuu wa Vituo vya Polisi na Maafisa Polisi Jamii wa Kata na kuwapatia maelekezo.
Miongoni mwa maelekezo aliyotoa RC Makalla ni pamoja na kamati za ulinzi na usalama ngazi ya wilaya kufanya kikao na wenyeviti wote wa mitaa usika ajenda ikiwa kudhibiti uhalifu.

Hata hivyo, RC Makalla ameelekeza Jeshi la Polisi kuanza msako wa kuwakamata wanunuzi wa mali za wizi huku akiwataka wakuu wa wilaya kuweka utaratibu mzuri wa kuanza kuwatumia askari mgambo katika kuongezea Nguvu Jeshi la Polisi.
Pamoja na hayo RC Makalla ametoa wito kwa Wananchi kuondoa hofu kwakuwa Serikali kupitia Jeshi la Polisi limejipanga kudhibiti uhalifu wowote.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam , Jumanne Muliro amesema jeshi hilo limejipanga kutekeleza maelekezo ya RC Makalla ambapo amesema tayari wanawashikilia watuhumiwa mbalimbali