NA DIRAMAKINI
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Viongozi kama ifuatavyo:-
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Viongozi kama ifuatavyo:-

Uteuzi huu unaanza tarehe 01 Juni, 2022.
Amemteua Mhandisi Cyprian John Luhemeja kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO). Mhandisi Luhemeja ni Mtendaji Mkuu, Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA).
Amemteua Bwana Macrice Daniel Mbodo kuwa Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC). Kabla ya uteuzi huo, Bwana Mbodo alikuwa Kaimu Postamasta Mkuu, Shirika la Posta Tanzania (TPC).
Uteuzi huu unaanza mara moja.