NA OR-TAMISEMI
KATIBU Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe ameipongeza timu ya mpira wa netiboli TAMISEMI Queens kwa kuibuka washindi wanne katika mashindano ya mchezo wa netiboli Afrika Mashariki yaliyofanyika katika viwanja vya Kamokya nchini Uganda hivi karibuni.
Prof. Shemdoe amesema kuwa ushindi huu haujapeperusha bendera kwa Ofisi ya Rais -TAMISEMI pekee bali kwa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania hususani katika nyanja ya michezo hivyo ameipongeza timu hiyo kwa kuwa wazalendo na kuiwakilisha vyema Tanzania na kuitaka timu hiyo kuendeleza jitihada ili kushiriki katika mashindano yajayo.
Pongezi hizo zimetolewa Mei 17,2022 katika viunga vya Ofisi ya Rais-TAMISEMI baada ya timu ya TAMISEMI Queens kuwasili ikitokea nchini Uganda kushiriki mashindano ya mchezo wa netiboli Afrika Mashariki ambapo timu ya TAMISEMI Queens ilifanikiwa kutinga katika hatua ya nusu fainali na kuibuka washindi wanne.
“Kwanza niwapongeze sana , mmekuwa wazalendo na mmewatuwakilisha vyema, lakini tumieni fursa hizi katika kukua sio kimichezo pekee lakini pia tumieni fursa hizi katika kukua kiuchumi,” Prof.Shemdoe.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhqWLAFsJZeK0aCaivA5hRc29mZiHPTHwQWromQwhoe9_i4nRXRjUz_KiGJf0x-KGXAV6ppUDbJED2sjGucbidR7cEiNqaEggUiTDrKoO0LvBqM66kAGxWIRwgwNlf1OIo7sXGdZp7K_HeRFJ9pVjHn3CEA0XbvmRMTx3clhAkX841jgPZ3Xks8LKYs/s16000/2.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj-1hSJN4ihgaWg0zafl7UzGD5A9RHLR3Twg4QLvi-WMii09lZKPQhRh_hQfXr0ZPYtb6DrXazxDShFBcXHNGixMBDxeWFf--Pwh16jGIcFZHrlQzuS0TXC9NMBVqt5Kp_q3siyttNzaKUL3lpPwyBhNsHuE31Iu0CosxzFFlOU0A35DgIHiNOCGUQW/s16000/1.jpg)