NA DIRAMAKINI
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) amepokea nakala ya Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Ethiopia nchini Mhe. Shibru Mamo Kedida katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.
‘‘Unaona timu yangu niliyoambatana nayo hapa, nichukue nafasi hii kukuhakikishia kuwa Wizara itakupa ushirikiano wote utakaouhitaji katika kutekeleza majukumu yako, saa 24 milango yetu iko wazi, tunataka uhusiano kati ya nchi zetu uzidi kuimarika,"alisema Balozi Mulamula.
Balozi Mulamula amesema Tanzania imefarijika kupata balozi mpya baada ya Balozi wa awali kumaliza muda wake wa uwakilishi, na kuongeza kuwa kitendo hicho ni ishara ya uhusiano mzuri na urafiki uliopo baina ya Tanzania na Ethiopia.
Naye Balozi Mteule wa Ethiopia Mhe. Sibru Mamo Kedida amemshukuru Waziri Mulamula kwa jinsi alivyompokea na kuelezea uhusiano kati ya Tanzania na Ethiopia ulivo mzuri na kuahidi kuwa atahakikisha uhusiano huo unazidi kukua na kuimarika.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhq_LY8maCEuEuln--FIcuaaO2IwjB-80SCVXrapMJbu1eOSOtFQUV8NQjcPiVFDYH9PZ57_sfMT2gVZwJeG-XaeuWYvB67TVtA-3fkcjabwfUBTjIUdDprgO0GyXsCIaFqIYrIdV6CQ5Z-ABPasT3PbWPFl9H60oa7KMqj6UT1dKHfKTn6nbK3WMXF/s16000/19.jpeg)
“Ethiopia na Tanzania zimekuwa katika uhusiano mzuri sana kidiplomasia, nchi zzetu zimekuwa na lengo moja, nitahakikisha uhusiano kati ya nchi hizi unaimarika na hata kufikia nchi hizi Tanzania na Ethiopia zinashirikiana kufanya biashara na uwekezaji kwa maslahi ya pande mbili,” amesema Mhe. Balozi Kedida.