NA MWANDISHI-WAF
WAZIRI wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu leo amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwenye kikao cha pili cha 'Global Covid-19' kwa njia ya mtandao ulioandaliwa za Serikali ya Belize, Ujerumani, Indoneaia, Senegal na Marekani.

Waziri Ummy amesema hadi sasa Tanzania imeshapokea dozi 11,232,374 kutoka COVAX facility pamoja na washirika wengine.
Vilevile Waziri Ummy ameeleza katika kikao hicho kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha wananchi wanapata Chanjo dhidi ya UVIKO-19 ikiwemo kutoa elimu ya umuhimu wa chanjo kwa kuwa hatujui wimbi jingine la Kirusi litakuaje.