NA DIRAMAKINI
SERIKALI kwa kushirikiana na Benki ya Uwekezaji ya Ulaya wanatekeleza Ujenzi wa Mfumo rahisi wa Maji taka kwenye makazi ya miinuko unaotekelezwa Bilioni 3.8 unaosaidia kuhifadhi maji taka kwenye matanki maalum na kuyatibu badala ya kumwaga kwenye Ziwa Victoria kama ilivyokua awali.


Vilevile,Mkuu
wa Mkoa ametoa wito kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka Halmashauri
ya Jiji la Mwanza kutoa elimu ya biashara kwenye vikundi vyote
wanavyowakopesha fedha kutoka makundi ya Wanawake, Vijana na wenye
ulemavu kwenye Halmashauri hiyo ili kuweka uhai wa vikundi
wanavyokopeshwa.

"Hawa wanafanya
vizuri ila mimi nimekuja kuona kama kikundi kina afya, je wana taarifa
za mapato na matumizi ya kikundi, wana vitabu vya fedha na wana
utaratibu wa kupima maendeleo ya kikundi chao, hapo lazima tujiulize na
Maafisa Maendeleo hiyo ndio kazi yetu kuwajengea uwezo", amesema.
Aidha,
Mkuu wa Mkoa amekagua Ujenzi wa Barabara ya Hesawa-Yatch Makaburini,
Tilapia -Vickfish yenye urefu wa Mita 650 liyotekelezwa kwa zidi ya
Milioni 348 na ameagiza kurekebisha dosari ndogo kwenye kingo za
barabara hizo na kusafisha mazingira.

Baada ya kukagua uhai wa Vilabu vya kupambana na rushwa na dawa ya kulevya katika shule ya msingi Nyegezi msafara wa Mhe Mkuu wa Mkoa ulifika kwenye Mradi wa Anuani za Makazi katika Mtaa wa Kisese kata ya Mkolani.
Kabla ya kukagua ujenzi wa jengo la Benki ya CRDB tawi la Buhongwa wenye thamani ya Milioni 500, Ujenzi wa Kituo cha Afya Bulale kata ya Buhongwa wenye thamani ya Milioni 500 umehitimisha ukaguzi wa miradi wilayani Nyamagana ambapo Mhe. Mkuu wa Mkoa amesisitiza ukamilishaji wa mradi huo kwa wakati ili uanze kuwahudumia zaidi ya wananchi elfu 5 wanaokusudiwa.