NA HAPPINESS SHAYO-WMU
SERIKALI kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeomba kibali cha kuajiri askari wa uhifadhi wapya 600 ambao watasambazwa kwenye maeneo hatarishi ili kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu.

Mhe. Masanja ameongeza kuwa Wizara ina mkakati wa kuanzisha vituo vya kikanda vya Askari katika maeneo yenye changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu.
Pia, amesema Serikali itatoa mafunzo kwa askari wa wanyamapori wa vijiji; na kuelimisha wananchi kuhusu namna bora ya kupunguza athari zinazotokana na wanyamapori wakali na waharibifu.
Katika hatua nyingine, akijibu swali kuhusu mikakati ya Serikali ya kutangaza maporomoko ya Kalambo Mhe. Masanja amefafanua kuwa Wizara itatumia vyombo vya habari, itaandaa machapisho na majarida na kushiriki katika maonesho, matamasha, matukio na makongamano ya utalii na biashara yanayofanyika ndani na nje ya nchi ili kutangaza kivutio hicho.
Pia amesema njia ya kuweka mabango katika viwanja vya ndege ikiwemo uwanja vya ndege wa Songwe na maeneo mengine katika Mkoa wa Rukwa itatumika kutangaza utalii huo.