NA SHEILA KATIKULA
WANANCHI mkoani Mwanza wameshauri kutumia mfumo mpya wa kidigitali wa Ni-Konekt kuomba huduma ya nishati ya umeme.

"Mfumo huu ni rahisi na unaokoa muda, kwani ukijaza taarifa zako kwa usahihi siku hiyo hiyo unafungiwa umeme,"amesema.
Amesema, mfumo huo unatumia njia tatu ikiwemo kupitia Ussd, web portal na mobile App.

"Mfumo huu umezinduliwa Juni 6, mwaka mpaka hivi sasa tumewaunganishia wateja wanne kwani Ni-Konekt ni huduma rahisi ambayo inarahisisha kupata umeme kwa urahisi na inapunguza urasimu na mianya ya vishoka,"amesema.



Moshi amesema mteja anaweza kutumia mfumo huo kwa simu maarufu kama kiswaswadu (kiganjani) simu janja,kompyuta,au kifaa chenye uwezo wa intaneti na kupata huduma.
"Kwa watumiaji wa Android inapatikana kwenye play store na App store kwa watumiaji wa Iphone,"amesema.

"Hatua zote za huduma hiyo zitafanyika kidigitali hadi kufikia hatua ya malipo na kulipia hatimaye kupatiwa huduma stahili haraka iwezekanavyo,"amesema Moshi.