NA SHEILA KATIKULA
WAHITIMU wa vyuo na vyuo vikuu ambao ni makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wametakiwa kutumia taaluma zao walizozipata vyuoni kwa kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo nchini ili kuleta maendeleo ya taifa kwa ujumla.
WAHITIMU wa vyuo na vyuo vikuu ambao ni makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wametakiwa kutumia taaluma zao walizozipata vyuoni kwa kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo nchini ili kuleta maendeleo ya taifa kwa ujumla.


"Inasikitisha kuona mtu anaelimu na ujuzi lakini amekata tamaa tumieni taaluma mliyoipata kwa kufanya kazi ili kuleta maendeleo".Hata hivyo aliongeza kuwa serikali inawasomesha watu ili wawe viongozi bora wa chama na taifa.

"Chama kimewandaa wanafunzi wa vyuo mbalimbali ambao wako ndani ya chama ili waje kuwa viongozi wajao watakaolitumiki taifa kwa masilahi ya maendeleo ya nchi,"amesema Hawasi.

Naye Katibu wa Seneti Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu, Salum Mtaturu amesema wameongeza idadi ya wanachana wa Chama Cha Mapinduzi kutoka 1400 na kufikia 2000 mpaka sasa.

"Tunaomba tuwezeshwe kadi 3000 za Jumuiya ya Vijana kwani itasaidia kuongeza wanachama na kuleta maendeleo, tunaomba tupewe miradi ili isaidie ruzuku kwenye shughuli za seneti,"amesema Mtaturu.