NA DIRAMAKINI
BEI ya mafuta imepanda tena mwezi huu na kuivuka ile ya Mei, iliyokuwa kubwa zaidi katika historia ya Tanzania kiasi cha kuilazimu Serikali kutoa ruzuku.
Mei, bei ya petroli ilifika shilingi 3,148 jijini Dar es Salaam ikipanda kwa shilingi 287 kutoka Aprili kwa kila lita moja huku dizeli ikipanda kwa shilingi 566 kutoka shilingi 2,692 hadi shilingi 3,258 katika kipindi hicho.
Katika taarifa iliyotolewa Julai 5, 2022 na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), bei ya rejareja jijini Dar es Salaam itakuwa shilingi 3,220 kwa lita moja ya Petroli na shilingi 3,143 kwa Dizeli huku mafuta ya taa yakifika shilingi 3,442.
EWURA imesema, bei hizi mpya ambazo zimejumuisha ruzuku ya shilingi bilioni 100 iliyotolewa na Serikali zinaanza leo, kama kusingekuwepo ruzuku hiyo lita ya petroli ingeuzwa shilingi 3,497 na dizeli shilingi 3,510 jijini Dar es Salaam wakati Kyerwa ingekuwa shilingi 3,735 kwa petroli na shilingi 3,748 kwa dizeli ambapo mafuta ya taa hayana ruzuku.
BEI ya mafuta imepanda tena mwezi huu na kuivuka ile ya Mei, iliyokuwa kubwa zaidi katika historia ya Tanzania kiasi cha kuilazimu Serikali kutoa ruzuku.
Mei, bei ya petroli ilifika shilingi 3,148 jijini Dar es Salaam ikipanda kwa shilingi 287 kutoka Aprili kwa kila lita moja huku dizeli ikipanda kwa shilingi 566 kutoka shilingi 2,692 hadi shilingi 3,258 katika kipindi hicho.
Katika taarifa iliyotolewa Julai 5, 2022 na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), bei ya rejareja jijini Dar es Salaam itakuwa shilingi 3,220 kwa lita moja ya Petroli na shilingi 3,143 kwa Dizeli huku mafuta ya taa yakifika shilingi 3,442.
EWURA imesema, bei hizi mpya ambazo zimejumuisha ruzuku ya shilingi bilioni 100 iliyotolewa na Serikali zinaanza leo, kama kusingekuwepo ruzuku hiyo lita ya petroli ingeuzwa shilingi 3,497 na dizeli shilingi 3,510 jijini Dar es Salaam wakati Kyerwa ingekuwa shilingi 3,735 kwa petroli na shilingi 3,748 kwa dizeli ambapo mafuta ya taa hayana ruzuku.

Mwezi uliopita, lita ya petrol iliuzwa shilingi 2,994 na dizeli shilingi 3,131 mkoani Dar es Salaam huku Kyerwa ikiwa shilingi 3,539 kwa petroli na shilingi 3,232 kwa lita ya dizeli.
Mwezi Juni