NA STEVEN NYAMITI-WM
WAZIRI wa Madini, Dkt. Doto Biteko ameupongeza mgodi wa dhahabu wa Buckreef kwa kutoa ajira kwa Watanzania wanaofanya kazi mbalimbali za uzalishaji wa dhahabu katika mgodi huo.
Dkt. Biteko amebainisha hayo Julai 16, 2022 wakati alipotembelea mgodi wa Buckreef mkoani Geita ili kujionea maendeleo ya shughuli za ujenzi na uchimbaji madini katika mgodi huo.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjmK-Q4kR5xfacn7LfBBw1esTyYpDJrTJttVfbhwn_2d8uCPCA4psXi0jS54L_VvokzMIMcBA1b3o9N-_wv5Hv6xm2Bs_wkSbVoC_Hs2Bs_ipb2IIuj_1BS8HHRDDOxdm8KnHi2g2MOEkznmzXaafNpXOZOlqFD7J0U__kZ1hrBjRL2_KVITYDBcBbIbQ/s16000/IMG-20220717-WA0040.jpg)
Amesisitiza kwa wafanyakazi waliopewa ajira katika mgodi huo kuhakikisha wanajenga taswira nzuri kwa kuwa wazalendo na waaminifu katika kazi zao.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgsN4o5kuCPLOp5mGW2r5Sn69CZ7GHHo26wggXphlMvuihCm7unZf4fPZwIKZe0R49EKYJVPJoQmJFVlZSQ9cPENKGOyfel8smz47lobLGHEpKNME7ih8u3DC7Vrqt2bXRr_4pnovEFtR_pC8TWvKKTENbudzQqfU1Fgguv81eOibm3TQfarzqawuKImg/s16000/IMG-20220717-WA0050.jpg)
Aidha, Dkt. Biteko amesisitiza kuwa, miradi yote iliyopo kwenye Sekta ya Madini itaendelezwa ili watanzania wanufaike na rasilimali madini na kuongeza Pato la Taifa.
"Matarajio ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ni kwamba miradi yote ambayo ipo kwenye Sekta ya Madini iweze kuendelezwa,"amesisitiza.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjeQoW7CbtV-aB3heYF494NEtRceAd1FWV16GxQs_Hp-pWUavZUXuUvVskLUT_Q__xahNoAOw3i0rgbe5kaW4f0HSdP5WdOdmgqpC3YNnW1gxBakrWGosODNenOq41ZZAvCV46MFcs3Mty8ILnsjkoMvH01Kl4t5wx-uXnBq1awMTyMDQhF2IWzQBoIMQ/s16000/IMG-20220717-WA0044.jpg)
Aidha, amemuomba Dkt. Biteko kuhakakisha Serikali inaleta wawekezaji wengi mkoani Geita kutokana na mkoa huo kuwa na maeneo mengi ya uwekezaji katika Sekta ya Madini.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj3LKAX41i1cOXg2SVnegfs4Mvb-59V28XkDUupxJqg2jc71Gjeh6ViR4Hr5L6MH5-rKx8uOuy1niRS8YckR-PCJpBcUMhBnCKrOasw2AVnrj72ucPNCtAnw-NkuB1UdtNrmI_nQI-wmhlva8FjO2dpEi7c69bF07jXdPq6oHCgKb8nk0NywMAZX1BMig/s16000/IMG-20220717-WA0054.jpg)
Aidha, shughuli nyingi za manunuzi ya vifaa mbalimbali yanafanyika hapa nchini ili kuhakikisha manufaa ya uwekezaji yanabaki kuwa ya watanzania.