NA FRESHA KINASA
SHIRIKA la Hope for Girls and Women in Tanzania (HGWT) linalojishughulisha na mapambano ya vitendo vya ukatili wa kijinsia lenye makao makuu yake Mugumu Wilaya ya Serengeti Mkoa wa wa Mara kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Wilaya ya Serengeti wameendelea na kampeni ya utoaji wa elimu kwa njia ya mikuano ya hadhara kuhusiana na madhara ya vitendo vya ukatili wa kijinsia katika kata za Rung'abure, Nyamoko na Geita Samo zilizopo wilayani humo.

Goodluck amewaomba wananchi waliopata elimu hiyo wawe mabalozi wa kutoa elimu hiyo kwa watu wengine. Huku akiwaomba wananchi kutowakeketa mabinti wakati wa likizo bali wawalinde sambamba na kushiriki kuhesabiwa Siku ya Sensa Agosti 23, mwaka huu.
"Niwaombe pia wazee wa kimila msaidie kumaliza ukeketaji, tumieni nafasi yenu kutokomeza ukeketaji. Mila ya ukeketaji haifai ina madhara makubwa kiafya, tuwalindeni watoto wa kike badala ya kuufanya ukejetaji kama njia ya kujipatia kipato zipo fursa nyingine nyingi ambazo zinaweza kusaidia kuingiza kipato kama vile kilimo, ufugaji, biashara, ujasiriamali na pia kutumia fursa ya kuunda vikundi kupata mikopo kutoka halmashauri hizi ni njia halali za kupata kipato na sio fedha ambazo zinatokana na malipo baada ya binti kukeketwa,"amesema Goodluck.
Sambamba na hatari ya kupata magonjwa ya kuambukiza kama UKIMWI kutokana na kutumia kifaa kimoja wakati wa kuketa, kuchangia ndoa za utotoni kwani binti anapokeketwa huandaliwa kuozeshwa, madhara ya kisaikolojia, kupoteza maisha kutokana na kutokwa damu nyingi pamoja na kutojiamini katika jamii.
Ameongeza kuwa, njia za kumaliza ukeketaji ni pamoja na kutekeleza sheria za ukeketaji kifungu namba 169( A ) kanuni ya adhabu iliyofanyiwa marejeo mwaka 2019 ambayo inatoa adhabu kuanzia miaka 5-15 pamoja na kulipa fidia kwa mhanga milioni moja hadi milioni tano.
Pia kutoa elimu kwa jamii juu ya madhara ya ukatili wa kijinsia, viongozi wa dini na vyama vya siasa kutoa elimu, kuwawezesha kiuchumi wanawake, kutoa elimu kwa umma kuhusiana na madhara ya ukatili wa kijinsia ukiwemo ukeketaji, mashahidi kufika mahakamani kutoa ushahidi ili waliokamatwa wakifanya vitendo hivyo wapewe adhabu kwa mujibu wa sheria.
Pia, SSGT Mufuluki amewaomba wananchi hao, kutoa taarifa mapema kabla binti hajakeketwa wanapoona maandalizi na viashilia mapema ili kuwaokoa kabla hawajafanyiwa vitendo hivyo huku akisema kila mmoja awe mstari wa mbele kupinga ukeketaji na aina mbalimbali za ukatili wa Kijinsia kwani ni kikwazo cha usawa katika Jamii na ustawi bora kwa maendeleo kuanzia ngazi ya familia.

Katika hatua nyingine, amewaomba wananchi hao kusisimamia maadili mema na malezi bora kwa watoto wao na kuwafundisha tabia njema sambamba na kufuatilia maendeleo yao ya kitaaluma katika kuandaa kizazi bora kitakacholeta mabadiliko chanya katika jamii na taifa kwa ujumla.


Ameongeza kuwa, wajibu wa muathirika wa ukatili wa Kijinsia ni pamoja na kwenda kutoa ushahidi mahakamani na pengine kumtambua mtenda makosa, kujua jina, anwani, na namba ya simu ya mpelelezi wake pamoja na maendeleo ya upelelezi wa Jambo alilolitolea taarifa, kutoa maelezo yake yote kwa Ofisa wa dawati la Jinsia na watoto bila kuficha Jambo lolote kwani atahakikishiwa usiri wa taarifa yake.
Pia CPL Sijali amesema, huduma ya Dawati kwa upande wa Watoto ni kuhakikisha watoto wanapata haki ya kulindwa dhidi ya aina zote za ukatili na unyanyasaji na kwamba endapo haki ya mtoto itavunjwa kosa hilo linatakiwa kutolewa taarifa haraka kwenye dawati la Jinsia na Watoto mara moja, na kwamba kila dawati linalenga kutoa mazingira rafiki kwa mtoto. Ambapo maafisa wa dawati watafanya kazi pamoja na Maafisa wa Ustawi wa Jamii ili kufuatilia kesi zinazohusu Watoto sambamba na kuwasaidia watoto wakati wa mahojiano na wakati wote wa hatua za mfumo wa haki kutokana na wao kuwa katika hatua za kutishika kurahisi.

Tags
Habari
HGWT
Jeshi la Polisi Tanzania
Kataa Ukatili
Mara
Serengeti
Unyanyasaji na Ukatili wa Kijinsia