NA DIRAMAKINI
WANANCHI wote walioomba nafasi ya kuwa Makarani na Wasimamizi wa Maudhui na Maofisa TEHAMA wametakiwa kuwa na subira kuhusu kutangazwa kwa majina ya watahimiwa watakaoshiriki kwenye usaili wa nafasi husika kwenye utekelezaji wa Sensa.


“Kuna watu wananung’unika kwanini hatutoi majina ya waliochaguliwa kuwa Makarani na Wasimamizi wa Sensa, Ofisi za Takwimu zinafuata utaratibu wa Kitaifa na Kimataifa na kuna ratiba yake ya kutekeleza Sensa,”amesema Makinda.
Sensa ya Watu na Makazi itafanyika tarehe 23 Agosti, 2022. Sensa kwa Maendeleo, Jiandae Kuhesabiwa.