NA DIRAMAKINI
MKUTANO maalum uliofanyika leo Julai 23, 2022 kuanzia saa 10 kamili hadi saa 12:30 jioni kwa njia ya ZOOM ukiangazia kukua kwa diplomasia ya uchumi na fursa za kiuchumi zinazopatikana katika nchi za Mashariki ya Kati na Asia umetoa picha na mwelekeo chanya kwa Watanzania ambao wana shauku ya kuvuka mipaka kwa ajili ya kupeleka biashara zao au kuwekeza katika maeneo mbalimbali duniani .

MHE.PROF GADIUS KAHYARARA KATIBU MKUU WIZARA YA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA
"Ili kurahisisha mfumo mzima wa kuhudumia hawa wawekezaji tumeona ni lazima tuwe na Digital Platform, ambapo mwekezaji kwa kutumia teknolojia ya kisasa akiwa na password moja anaweza kupata zile huduma zote ambazo anatakiwa kwa ajili ya uwekezaji.

SHARIFF A. SHARIFF MKURUGENZI MTENDAJI WA MAMLAKA YA KUKUZA UWEKEZAJI ZANZIBAR (ZIPA)

"Uchumi wao ni uchumi ambao kwa kweli kwa vyovyote vile tunahitaji Tanzania na mashirikiano hayo kupitia Economic Diplomacy ndipo tunaweza kufanya wao kuleta ama sisi kupeleka bidhaa kwao,"amesema.
BALOZI MHE. ANISA K. MBEGA BALOZI WA TANZANIA NCHINI INDIA


BALOZI MHE. BARAKA H. LUVANDA BALOZI WA TANZANIA NCHINI JAPAN
"Kazi kubwa kama Balozi ni kutekeleza Diplomasia ya Uchumi kwa kuitangaza Tanzania kama ni sehemu sahihi kwa wawekezaji, wafanyabiashara na watalii kutoka nchi hizo tunazosimamia.

"Katika kutekeleza Diplomasia ya Uchumi majukumu muhimu ambayo tunayasimamia ni kuvutia wawekezaji wa Japan, kutafuta masoko ya bidhaa za Tanzania nchini Japan, misaada na mikopo ya masharti nafuu kwa miradi ya maendeleo ya Tanzania,"amesema.
BALOZI MHE. MOHAMMED MTONGA BALOZI WA TANZANIA NCHI ZA KIFALME ZA KIARABU
"Ni moja ya nchi zenye uchumi mkubwa na zenye rasilimali kubwa na sisi kama Balozi wajibu wetu mkubwa sasa hivi ni kuvutia mitaji na wawekezaji kuja kuwekeza Tanzania na Hali kadhalika kuona fursa ambazo zipo Tanzania tunaweza kufanya biashara Ili tuwe sehemu ya mafanikio ya UAE.
"Uwekezaji uliopo katika nchi za Falme za Kiarabu hasa hasa katika kitovu cha biashara nazungumzia Dubai ni karibu nchi nyingi za Dunia zinalitazama eneo hili kama Strategic Position ya kuwekeza mitaji yao kwa hiyo unapofanya biashara na UAE ujue unafanya biashara na Dunia.
BALOZI MHE. ALI JABIR MWANDINI BALOZI WA TANZANIA NCHINI SAUDI ARABIA


"Saudi Arabia ni wadau wakubwa sana wa sekta ya afya na wamekuwa wakituma madaktari bigwa kuja Tanzania kushirikiana nasi katika hospitali ya moyo ya Jakaya Kikwete, lakini pia mwaka huu mwezi Septemba watakuja Zanzibar kwa mara nyingine.

BALOZI MHE. DR. RAMADHANI KITWANA DAU BALOZI WATANZANIA NCHINI MALAYSIA