NA MWANDISHI WETU
WAZIRI Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa ameweka jiwe la msingi katika Kituo cha Afya Mtoa kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mkoani Singida mara baada ya kufanya ziara yake ya kikazi wilayani humo.

Miundombinu inayojengwa katika kituo hicho ni pamoja na jengo la Mama na Mtoto, Maabara, jengo la upasuaji, chumba cha kuhifadhia maiti, nyumba ya mtumishi na jengo la kufulia.