NA MWANDISHI WETU
SERIKALI kupitia Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari pamoja na taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo zimeendelea kuboresha upatikanaji wa huduma za Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa jamii ya wafugaji wa kijiji cha Msomera kilichopo Handeni, Tanga ambao ni wakaazi wapya waliohamia kwa hiyari katika kijiji hicho wakitokea katika eneo la hifadhi ya Ngorongoro

“Tutahakikisha upande wa mawasiliano hakuna changamoto tena katika kijiji hiki cha Msomera, tutaendelea kuratibu kadiri ambavyo wananchi wanaendelea kuongezeka katika kijiji hiki ili kila mmoja apate huduma bora za mawasiliano ya simu, redio, televisheni pamoja na Anwani ya Makazi ili waweze kushiriki katika uchumi wa kidijiti,”amesisitiza Dkt.Yonazi.




Akizungumza katika ziara hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Mhandisi Peter Ulanga amesema kuwa ifikapo Julai 14, 2022 huduma za mawasiliano ya TTCL zitaanza kupatikana katika kijiji hicho lakini pia hadi mwishoni mwa mwezi Julai huduma za mawasiliano za kampuni za Tigo, Airtel, Halotel na Vodacom zitakuwa zinapatikana katika kijiji hicho ambapo wataweka vifaa vyao katika mnara huo.

Naye Mwenyekiti wa kijiji ncha Msomera, Bw. Martine Oleikai Paraketi ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia kwa kuamua kuboresha sekta ya elimu kwa kuwezesha wanafunzi wa kijiji cha Msomera kujifunza kupitia vifaa vya TEHAMA na intaneti kuanzia shule ya msingi na Sekondari na wana imani kuwa Msomera itazalisha wasomi wengi.
