NA FRESHA KINASA
MBUNGE wa Jimbo la Musoma Vijijini mkoani Mara, Prof.Sospeter Muhongo amewataka wananchi wa jimbo hilo kujitokeza kushiriki kikamilifu kuhesabiwa siku ya Sensa ya Watu na Makazi ambayo itafanyika Agosti 23,mwaka huu.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi_96SuJlPpd_AiGDYODsjfc_fWCW9HJ-2rrNN4UtbuDZ40JhdUBmYLSWeQovpib7NHrYoekaUQ9BI3v-Xdh0FcDJySIAxzpUbyZezzwxA5W1FDTPajZ5ROZ4fR3YohGJxXIlGB4i6b3fXDaxIWCzokMrQpY3UcimMsuEwQFUapmRTp6KCFlS5CsHBzdg/s16000/IMG-20220730-WA0227.jpg)
Amesema kuwa, kwa msingi huo sensa ni zoezi muhimu ambalo kila mmoja kwa nafasi yake analazimika kushiriki na kutimiza wajibu wake ili kuhakikisha inakuwa na mafanikio makubwa katika kuisaidia Serikali kutimiza wajibu wake kwa wananchi kulingana na idadi ya watu wa eneo husika ikiwa kama msingi mkubwa wa utoaji wa maendeleo kwa kila eneo la utawala hapa nchini.
Ameyasema hayo leo Julai 30, 2022 wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji na uelimishaji jamii juu ya Sensa ya Watu na Makazi iliyofanyika Busekera katika Kata ya Bukumi Wilaya ya Musoma Mkoa wa Mara na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, viongozi wa dini, chama pamoja na wananchi.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjdI5MVR7XgvWmhCemY32jWRvPYG0KTLCOGoCdfONuwuzajrkj_35u_IQdpzkxdx3t3bp4KvXXgtP5psW_P67HtGsIu6BRKi6_69H_cFLHdRg7vooYUlFHUz1Nv1fqY1PyDxLB4jF5nOCItGs7LFanaGEXa1r05L3QrwlV8Z9gid_fr941TLrYpnN55Dg/s16000/IMG-20220730-WA0230.jpg)
"Musoma vijini tuna shule 111 za msingi, shule shikizi 5, sekondari 21, tunajenga shule nyingine 10 na maabara zinajengwa sekondari zote. Tunayo High School moja tu nimepeleka maombi serikalini naulizwa tunataka high school tuko wangapi? Nashindwa kutoa takwimu sahihi, niwaombe wananchi kusudi serikali iendelee kupanga mipango ya maendeleo na kutuletea maendeleo kwa usahihi sote tuhesabiwe siku ya sensa ili tutambulike. Mwambie ndugu yako aliyeko nyumbani ahesabiwe kwa faida yake na jimbo letu," amesema Prof. Muhongo.
Aidha, Prof.Muhongo amewataka wananchi wa jimbo hilo kutowaficha ndani watu wenye ulemavu badala yake wahesabiwe siku ya sensa. Huku akisema atapita kila kijiji kufanya hamasa na kutoa elimu juu ya umuhimu wa sensa ili watu wote ndani ya jimbo hilo wahesabiwe.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjafvf9jVa5SDHA7dmG8p5VjRdiGf7JLLCYHsuSC-DvsKwJrNIg0liPOWaiLQqOijhaTfg0aIOgIfcb8b2aSs7N9wa8HcZMc7oFo3zIpxKA27kWEiVNyPN-BXp8ltihKetT3JLhQ7_z7lIGRMOVOlN0dNZR9Gh9mCa7gXSYDg0i50_3E0Joleavny4MeQ/s16000/IMG-20220730-WA0228.jpg)
"Watauliza pia kiwango chako cha elimu, shughuli zako, taarifa za ulemavu, hali ya uzazi, taarifa za umiliki wa ardhi, taarifa za vifo na vifo vitokanavyo na uzazi, hali ya nyumba, anwani za Makazi, taarifa kuhusu Mpango wa TASAF, umri, jinsi, hali ya ndoa, taarifa za uhamiaji, taarifa za vitambulisho vya taifa na uhai wa Wazazi, taarifa za majengo niwaombe toeni taarifa kwa ushirikiano wa dhati kufanikisha Jambo hilo muhimu kwa nchi yetu,"amesema Dkt.Haule.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh2DcLuGO37UaZjKUK0iLh247PET3OC_OY77RotVc2GE85j5C0GUlZSqSbP4EdjnuFrSbraYB-E7Pv2-8tLbfNjfhlHYbHx0eyDe2_ymn0tQrBqTxC64f3Fw_9DLMjmBv7u9Mr0cSd4K64SBU2kshXe7i7KcLm10-uFXaUOE-QcB3rFPenczs8cEpic7w/s16000/IMG-20220730-WA0232.jpg)
Diwani wa Kata ya Bukumi, Munubi Mussa amesema kuwa, wananchi wa kata hiyo wamejiandaa kushiriki kwa ufanisi kuhesabiwa.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh2IqPy6as2MTia5mSOdh9i7onQdxK3GFIP_14xnTejgxKovj7BYQYwFVCNGaARIewSbxAflyFuJJZRBEvEPhvu4cKtjCOxn8M4jGLvFf45tFfl73zGghkaVF1xZ699RIqEPNwOxloNj1FpnU3v-pN0-eWdu4gURjWdx3OOLyUxa8ovwTW1hgb9m7F-TA/s16000/IMG-20220730-WA0231.jpg)
Charles Magoma ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Musoma ambapo amesema kuwa, maendeleo yote yanayofanywa na Serikali yanatokana na Wananchi hivyo watimize wajibu wao kuhesabiwa.