NA MWANDISHI WETU
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu, Mhe. George Simbachawene amepongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma kwa kutekeleza vizuri zoezi la anwani za makazi.

“Uwekaji wa anwani za makazi unaenda sambamba na zoezi la sensa ili kujua katika ramani mahali mitaa, barabara zilipo. Mmefanya jambo zuri ambalo watu wengine wanapaswa kuja kujifunza alisema waziri;

“Haya ni maelekezo ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ambaye aliagiza operesheni ya postikodi ili watanzania wajulikane wanakaa wapi; jambo la kuweka mitaa, lakini pia barabara na namba kwenye nyumba katika Halmashauri Wilaya ya Mpwapwa na jimbo la Kibakwe limefanyika kwa mazingira makubwa;
