NA MATHIAS CANAL
SERIKALI imesema kuwa, imeamua kufanya mageuzi ya elimu ambapo kufikia mwezi Disemba 2022 rasimu ya mitaala mipya pamoja na rasimu ya mapitio ya sera itakuwa imekamilika.

Serikali ya Tanzania imejipanga vyema na kufikia mwezi Januari mwaka 2023 inatarajia kuanza mchakato wa kufanya maamuzi baada ya rasimu hiyo kuwa imekamilika.
Pamoja na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.Prof Adolf Mkenda mkutano huo pia umehudhuriwa na Waziri wa Elimu wa Namibia, Mhe. Ester Anna Nghipondoka, Naibu Waziri wa Elimu Bosnia na Herzegavina, Adnan Husic, Mkurugenzi wa Idara ya Masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa na Katibu wa Tume ya Kitaifa ya Elimu ya Qatar ya Utamaduni na Sayansi,Ali Al-Marafi.
