NA MWANDISHI WETU
WAZIRI wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Mhe Dkt.Ashatu Kijaji (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba, Mhe. Bruno Rodriguez Parrilla kuhusu uwezekano wa kupanua zaidi kiwanda cha kuzalisha viwatilifu ili kuzalisha bidhaa ya mbolea pamoja na bidhaa zingine za afya.

"Kilimo ni sekta ambayo inachangia kwa kiwango kikubwa kwenye uchumi wa Taifa letu hivyo mbolea ni moja ya ya malighafi muhimu kuhakikisha kilimo kinakuwa na mchango mkubwa kwenye uchhumi wa Taifa letu, sisi kama Wizara tuko tayari kuhakikisha kiwanda chetu kinaendelea na uuzalishaji wa bidhaa hizi muhimu kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu,"amesema Waziri Kijaji.
Aidha, Waziri Kijaji amesema majadiliano kati ya Serikali ya Tanzania na Cuba yanatarajiwa kuanza hivi karibuni na timu za wataalamu kwa nchi zote mbili zimeundwa na zipo tayari kuanza majadiliano mara baada ya wataalamu kutoka cuba kuingia nchini kuanzia Julai 8 hadi 10, mwaka huu.

"Uhusiano wetu na Cuba ni mzuri na unaendelea kuimarika siku hadi siku na tutaendelea kushirikiana kwenye sekta mbalimbali hususani kwenye sekta yya afya,Elimu pamoja na Viwanda,"amesema Balozi Mlowola.
Tags
Diplomasia ya Uchumi
Habari
Kituo cha Uwekezaji Tanzania
Tanzania and Cuba
Uhusiano wa Kimataifa
Wizara ya Uwekezaji na Biashara