NA DIRAMAKINI
IMEELEZWA kuwa, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na watu wake wana nafasi kubwa ya kuzitumia fursa za kiuchumi zilizopo nchi za Bara la Ulaya kunufaika kiuchumi, kutokana na misingi mizuri ya uimarishaji wa diplomasia ya uchumi iliyowekwa na Serikali.

Ni kupitia mkutano muhimu na maalum ulioratibiwa na Watch Tanzania kupitia Mtandao wa Zoom ambapo umeangazia juu ya KUKUA KWA DIPLOMASIA YA UCHUMI NA FURSA ZA KIUCHUMI ZINAZOPATIKANA NCHI ZA BARA LA ULAYA. Washiriki wa mkutano huo wamesema;
BALOZI MHE. ASHA-ROSE MIGIRO BALOZI WA TANZANIA NCHINI UINGEREZA
"Uingereza imekuwa mshirika mkubwa sana wa maendeleo katika nchi ya Tanzania, kwani imeweza kusaidia na kushirikiana na Serikali yetu katika utimilifu wa miradi mbalimbali ikiwemo sekta ya ujenzi, sekta ya kilimo na ufugaji na hata Sayansi na Teknolojia;


BALOZI MHE.GRACE ALFRED OLOTU, BALOZI WA TANZANIA NCHINI SWEDEN
"Sweden ina miradi nchini Tanzania isiyopungua 200 kutoka makapuni mbalimbali, miradi hiyo ina thamani ya dola za Kimarekani milioni 726.63 na inachangia ajira za moja kwa moja zipatazo 15,191;

BALOZI JESTUS NYAMANGA, BALOZI WA TANZANIA NCHINI UBELIGIJI
"Moja ya faida ya kibiashara ambayo Watanzania wanaweza kunufaika nayo ni kwamba nchi yetu Tanzania inauza sana bidhaa nchini Ubeligiji kuliko tunavyonunua, kwani mwaka jana tuliuza bidhaa za Euro millioni 75.2 na wao waliuza bidhaa za Euro milioni 72.5;

BALOZI MHE. SAMWEL SHELUKINDO, BALOZI WA TANZANIA NCHINI UFARANSA
"Ndani ya hii miaka miwilii Shirika la Maendeleo la Ufaransa limeweza kuongeza misaada zaidi kwa masharti nafuu kutoka Euro milioni 100 kwa mwaka kufikia milioni 150;
1. Miradi ya kimkakati (SGR, JNHS n.k)
2. Uchumi wa bluu Zanzibar na Usalama wa bahari kuu
3. Usafirishaji wa mizigo
4. Ujenzi wa kiwanja cha ndege Terminal 2 ,"amesema Balozi Shelukindo.
BALOZI MHE.MAIMUNA TARISHI BALOZI MWAKILISHI WA KUDUMU UMOJA WA MATAIFA (UN), GENEVA, USWISI
"Kupitia ziara mbalimbali za viongozi wetu wameweza kushiriki mikutano mbalimbali ya mashirika ya Umoja wa Mataifa na kupata fursa mbalimbali ikiwemo kupokea dola za kimarekani takribani milioni 3.5 ambazo ni sawa na bilioni 7 za kitanzania, ambazo sio mkopo zilitolewa na Shirika la Biashara Duniani (WTO) kwa ajili ya kuongeza thamani za mbogamboga na matunda nchini;

BALOZI DKT.ABDALLAH POSSI BALOZI WA TANZANIA NCHINI UJERUMANI
"Utalii ni moja ya fursa kubwa sana kwa nchi ya Ujerumani kuja Tanzania, kwani kutokana na kipindi cha Low na High Session tunategemea 2023 watalii watakuja zaidi ya 90,000 kwa mwaka;

BALOZI YACOUB MOHAMMED, BALOZI WA TANZANIA NCHINI UTURUKI
"Ziara ya Mhe.Rais wa Uturuki Tayyip Erdoğan mwaka 2017 nchini Tanzania iliibua masuala mengi pamoja na kufunguliwa ubalozi wa Tanzania nchini Uturuki na kuzidi kuimarisha diplomasia kwa nchi zote mbili;

BALOZI CELESTINE J. MUSHI BALOZI WA TANZANIA NCHINI AUSTRIA
"Diaspora ya hapa nchini imenisaidia sana kujua uongozi na viongozi wa hapa na kujadili ni kwa namna gani tunaweza kukuza uhusiano wetu na nchi ya Austria na kuchangamkia fursa zilizopo, kwani Ubalozi wetu bado ni mchanga.
"Kutangaza fursa zinazopatikana nchini Austria moja ya nyenzo ni kutumia Watanzania walioishi hapa nchi hii kwa muda mrefu (Diaspora), hivyo nilivyofika nilianza kuandikisha Watanzania waishio Austria na idadi yake kuwa 118," amesema Balozi Mushi.