NA FRESHA KINASA
WANANCHI wa Kata ya Makojo Wilaya ya Musoma Mkoa wa Mara, wamemuahidi Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini ambaye ni mbunge wao kuwa, wamejitayarisha kwa asilimia 100 kuhesabiwa siku ya Sensa ya Watu na Makazi Agosti 23, 2022 baada ya kupata elimu na hamasa thabiti ya umuhimu wa sensa kutoka kwa Mbunge wao Mheshimiwa Prof. Sospeter Muhongo.
Kata ya Makojo inaundwa na vijiji vitatu Chimati, Chitare, na Makojo ambapo wananchi hao walitoa ahadi hiyo Agosti 13, 2022 wakati Mbunge Prof. Sospeter Muhongo alipokuwa ndani ya kata hiyo akifanya ushawishi, hamasa na kutoa elimu kwa wanavijiji wa kata hiyo ambapo aliwaambia wao pamoja na wageni wao washiriki kuhesabiwa siku hiyo ya Agosti 23, 2022.
Wakati wa majadiliano ya kila kaya na kila mwananchi kuhesabiwa Mbunge Mheshimiwa Muhongo aliwakumbusha wananchi wa kata hiyo kuwa vipaumbele vya kata yao ni pamoja na elimu, afya, kilimo, uvuvi, vinavyohitaji ushiriki na uchangiaji wa Serikali.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi5cPR2HD1vC8JAiXk3hK-_GVnBE59YVix-tlXs4JJTZRAMTHWJTt2z3y761rwLMbx37Ct9T8Ckxj2RFxg46Pn9lNlyyxgGcxjDY48TCgqgv9KS5Nsddb9HLC0lF7bg4dASdLv3WebA_9rC7o8RNNn6IrFfUu_0n2atKo_WjR-U_5UqFGMoOZRXuN68tw/s16000/IMG-20220816-WA0244.jpg)
Kufuatia elimu hiyo iliyotolewa na Mheshimiwa Prof.Muhongo wanavijiji wa Kata ya Makojo wanao uelewa mkubwa juu ya umuhimu wa kuhesabiwa na wanakubali kwamba takwimu sahihi zinahitajika sana kwa mipango mizuri sana ya miradi yao ya maendeleo. Hivyo kama zilivyo kata nyingine 20 za Jimbo la Musoma Vijijini watahesabiwa wote kwa asilimia 100.
Aidha, miradi ya kata ya Makojo ambayo imekwisha pokea fedha kutoka serikalini ni ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Makojo na shilingi milioni 500 zimekwishatolewa huku viongozi na wananchi wao wakiishukuru Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kutoa fedha za Mradi huo muhimu sana kwao.
Mradi mwingine ni wa Maji wa bomba ya Ziwa Victoria ambao una thamani ya Shilingi Bilioni 1.072 ni wa kusambaza maji ya bomba kwenye vijiji vya Chitare na Makojo ambao ulianza kwenye mwaka wa fedha 2013/2014 umechelewa kukamilika na ulisimamiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Ambapo RUWASA inajitahidi kurekebisha kasoro zilizopo.
Huku, wananchi wakiwa na imani kubwa na serikali sambambana na Mbunge wao Mheshimiwa Muhongo kwamba mradi huo utakamilika wananchi waanze kupata huduma ya maji Safi na salama kwani ni dhamira ya serikali kuhakikisha huduma ya maji inaimarika kwa kiwango stahiki.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgu6pX3n1LkiGfd5Z3sxvV1YURHC86X-cq31MsHOjbj1q-k5JZf2q0X0yFvxUjToTU2Zx_0HOW34tClrpr4hj9f9S9bVeNElCZWHksauR25KUEBlYwTZVR4oCX-HlqgxyMJ4M9zYBqzuObhgpOXjcKZ3og-flK4gia3RLjDHzOSQ4ElFLyXRjNPI745XA/s16000/IMG-20220816-WA0249.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiKYpo1A4ILvtZmneVe6_rqkwtxJvPbIN5tnYJ_4VIJVd3o1VQgr95AcyvhlQaPm7vW1tetqfwX2_tB9xTzxY4_W1mfw2zEUgxyduxxRdsGxO097w_wc1tUoYywP-VqW3bHM6fzwwMLXaZIMNpNb5oiFcu6-nZsAV78kgKrmWzAscQ2e_eO2Mw7ufiHYA/s16000/IMG-20220816-WA0246.jpg)
Kuhusu miradi ya TARURA ndani ya kata ya Makojo, TARURA imekamilisha na inaendelea kubooresha eneo la Makojo- Chitare- Kurugee na Chitare - Mwikoko- Rusoli. Ambapo barabara hizo ni muhumu sana kwa uimarikaji wa uchumi wa Wavuvi na Wakulima wa eneo hilo.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhZRktdcGhqQPKk0u5mZKhSjNHO36HggQ35PdOGngbfDCooLI4if7Bqz8SIiqz0BzJruIbZJSYA5E7wzuJ30-HCtO_Bb8jVU1HmmSr5Mfi7ZgRugczLLrhtwPESnI1L-soz8N2RP-5MYi6NQ138pNliA_jc4nrYdro4st2824WKDJUDmWCHAQMrWhjLYg/s16000/IMG-20220816-WA0247.jpg)
Mradi wa tatu ni ujenzi wa Makojo-High school Wanavijiji wamemuomba Mbunge wa Jimbo lao Mheshimiwa Prof. Muhongo ashirikiane nao kwenye ujenzi wa High School hiyo. Ambapo Mbunge amekubali ombi hilo na kikao Cha mradi huo kitafanyika mwishoni mwa mwezi Septemba 2022.