NA MWANDISHI WETU
WAZIRI wa Nishati Mhe.January Makamba amekutana na Mhe. Balozi wa Oman nchini Tanzania Mhe. Saud Hilal Al Shidhani na kuzungumzia fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo katika sekta ya mafuta na gesi hususani katika miradi mikubwa inayoendelea kutekelezwa nchini.
.jpg)
Kupitia Mazungumzo hayo Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) litashirikiana na Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Oman (OQ) kufanya biashara ya mafuta ya jumla (fuel supply), kujenga vituo vikubwa vya gesi za mitungi (LPG) na kushirikiana na Kampuni Tanzu ya TPDC (TANOIL) ili kufanya biashara ya rejareja ya mafuta.

Waziri wa Makamba wakati wa mazungumzo hayo amesema Tanzania inatafuta Washirika wa kimkakati ambao watashirikiana na TPDC katika kutafuta mafuta na gesi katika vitalu vilivyopo ili kuchochea ukuaji wa viwanda na kuongeza ukuaji wa uchumi nchini hususan katika miradi ya kimkakati ukiwemo wa Mwalimu Julius Nyerere.

Aidha, amesema Oman ina ujuzi mkubwa katika masuala ya mafuta hivyo amemhakikishia Waziri Makamba kuwa watashirikiana vyema katika kukuza sekta hiyo nchini Tanzania.