NA MWANDISHI WETU
KATIBU mstaafu wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) ambaye kwa sasa ni mjumbe wa jukwaa hilo, Bw.Neville Meena amesema kuwa, Sheria ya Vyombo vya Habari ya Mwaka 2016 ilikataliwa siku ya kwanza baada ya kusainiwa na kuanza kutumika kama mwongozo kwa vyombo vya habari nchini.
KATIBU mstaafu wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) ambaye kwa sasa ni mjumbe wa jukwaa hilo, Bw.Neville Meena amesema kuwa, Sheria ya Vyombo vya Habari ya Mwaka 2016 ilikataliwa siku ya kwanza baada ya kusainiwa na kuanza kutumika kama mwongozo kwa vyombo vya habari nchini.

“Sheria ya Habari ya Mwaka 2016 ilipingwa na wadau wa habari siku moja baada ya kupitishwa ili kutumika. Si kwamba, hakukuwa na vitu muhimu kwa wanahabari, wadau waliona imebeba mitego na madhara mengi kwa wanahabari na vyombo vya habari,’’amesema Meena.
Amesema, kutokana na yaliyomo kwenye sheria hiyo, wadau wa habari waliamini vyombo vya habari vitazidi kusinyaa.
‘‘Wadau wa habari wakiwemo UTPC, TAMWA, MISA-TAN, LHRC, TLS, Twawezaa, Sikika, THRDC na wengine, walikaa pamoja na kuangalia madhara yanayoweza kutokea kutokana na sheria hiyo.
‘‘Tunashukuru hatua zilipofika kwa sasa. Rais (Samia Suluhu Hassan) amekuwa na utashi wa kufanya mabadiliko lakini hata waziri aliyepo sasa (Nape Nnauye), mwelekeo wake ni huo,’’amesema Meena.
Amesema, baada ya serikali kuona umuhimu wa kupitia sheria hizo, iliandaa maboresho na kupeleka kwa wadau kupitia.
Pia amesema kwamba, baada ya wadau kupata mapendekezo hayo, waliyapitia na kuongeza pia kupunguza huku wakipitia zaidi vifungu vingine vya sheria vilivyoonekana kuwa hatari kwa wanahabari kutekeleza majukumu yao.
‘‘Hata yale mapendekezo yaliyoletwa na serikali, nayo tuliyaangalia na kuyapitia kisha kukubalina na baadhi na kisha mengine kutokubaliana nayo.

Ametaja eneo lingine lenye ukakasi kuwa ni matangazo ya serikali kuratibiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo.
‘‘Sasa hapa ni kuwa, kama Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo haelewani nawe ama chombo chako, huwezi kupata matangazo. Tukumbuke uchumi wa vyombo vya habari ni matangazo,” amesema Meena.