NA STEVEN NYAMITI
SERIKALI kupitia Wizara ya Madini inatarajia kuanzisha mashindano ya mchezo wa mbio utakaojulikana kama ‘Tanzania Madini Marathon’ ifikapo Mwaka 2023 ili kuhamasisha watanzania kushiriki katika michezo maeneo mbalimbali nchini.
Aidha, Dkt. Biteko amesema mwaka 2023, Serikali itaifanya Tanzania Madini Marathon kuwa ya kitaifa kwa kuwakutanisha wadau wa Sekta ya Madini na Sekta nyingine ili kushiriki kwa pamoja.
Vile vile, ametumia fursa hiyo kumpongeza Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Sophia Mjema kwa kuandaa vizuri Shinyanga Madini Marathon ambayo imekuwa ya kwanza hapa nchini kuanzishwa.
Naye, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mjema ameipongeza Wizara ya Madini kwa kushirikiana pamoja katika shughuli hiyo katika mkoa huo. Amesema kupitia marathon hiyo imeweza kuweka ukaribu wa Serikali na wananchi katika kufanya mazoezi ili kujenga mwili.
Wazo zuri sana hilo
ReplyDelete