NA MWANDISHI WETU
NAIBU Waziri wa Maji Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) ametembelea eneo hilo na kushuhudia Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani wakiendelea na uchimbaji wa visima viwili. Mheshimiwa Mahundi amesema utekelezaji huo ni katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya majisafi karibu na makazi yao.
NAIBU Waziri wa Maji Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) ametembelea eneo hilo na kushuhudia Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani wakiendelea na uchimbaji wa visima viwili. Mheshimiwa Mahundi amesema utekelezaji huo ni katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya majisafi karibu na makazi yao.

Amewataka wananchi wa Same kuendelea kuiamini serikali kwani Rais Samia Suluhu Hassan ambaye amejipambanua kama mama ambaye anatambua changamoto wanayo kutana nayo wakina mama wenzake hapa nchini.
Kwa upande wake Mkurugenzi Bodi ya Maji Bonde la Pangani Segule Segule amesema visima hivyo vinavyochimbwa vitakuwa na urefu wa zaidi ya mita 250 kila kimoja, lengo ni kuhakikisha maji yanayopatikana yanatosheleza mahitaji ya wananchi walio wengi.